Educationnewshub.co.ke
KISWAHILI REVISION NOTES
SEHEMU YA KWANZA- MASWALI NA MAJIBU

 

  1. Chagua mojawapo ya mazao yafuatayo na ueleze uzalishaji wake tangu kutayarisha shamba hadi kuvunwa.
  • Mahindi
  • Nyanya

 

  1. Ganga ganga za mganga humlaza mgonjwa na matumaini.

 

  1. Siku yangu ya kwanza katika shule ya upili.

 

  1. Andika insha itakayomalizia kwa maneno yafuatayo:

” … dunia kweli wakati wa sasa imefikia kilele cha maendeleo ya teknolojia.”

Download more free unlimited Kiswahili resources here: Educationnewshub.co.ke

KISWAHILI USHAIRI NOTES WITH EXAMPLES AND GUIDES

Kiswahili Fasihi, English Literature Notes, Guides, Revision Questions (Kigogo, Chozi La Heri, Blossoms, Tumbo, A Doll’s House, Inheritance)

Free Kiswahili Fasihi notes, Ushairi notes, isimu Jamii notes and Many More: Mwongozo wa kigogo, Kidagaa, Tumbo lisiloshiba, Chozi..

Bembea Ya Maisha Mwongozo Free Kiswahili Notes For Secondary Schools Free Downloads

KISWAHILI NOTES- REVISION KIT

Kigogo Kiswahili setbook free Guides, KCSE Questions and Answers Downloads

Free Kiswahili notes, revision questions, KCSE past Papers, Exams, Marking Schemes, Topical revision materials, Syllabus and Many more

Kiswahili free lesson plans for all topics (Form one to four)

KISWAHILI LUGHA NOTES FORM 1, 2, 3 & 4

Kiswahili Topic By Topic Questions And Answers PAPER 1-3 (All Topics)

KCSE Set Books Revision Questions and Answers (English and Kiswahili)

Free Kiswahili Notes, Exams, Schemes of Work, Lesson plans and other revision materials
Free Kiswahili Notes, Exams, Schemes of Work, Lesson plans and other revision materials

KISWAHILI I

SEHEMU YA PILI:

Download more free unlimited Kiswahili resources here: Educationnewshub.co.ke

KISWAHILI USHAIRI NOTES WITH EXAMPLES AND GUIDES

Kiswahili Fasihi, English Literature Notes, Guides, Revision Questions (Kigogo, Chozi La Heri, Blossoms, Tumbo, A Doll’s House, Inheritance)

Free Kiswahili Fasihi notes, Ushairi notes, isimu Jamii notes and Many More: Mwongozo wa kigogo, Kidagaa, Tumbo lisiloshiba, Chozi..

Bembea Ya Maisha Mwongozo Free Kiswahili Notes For Secondary Schools Free Downloads

KISWAHILI NOTES- REVISION KIT

Kigogo Kiswahili setbook free Guides, KCSE Questions and Answers Downloads

Free Kiswahili notes, revision questions, KCSE past Papers, Exams, Marking Schemes, Topical revision materials, Syllabus and Many more

Kiswahili free lesson plans for all topics (Form one to four)

KISWAHILI LUGHA NOTES FORM 1, 2, 3 & 4

Kiswahili Topic By Topic Questions And Answers PAPER 1-3 (All Topics)

KCSE Set Books Revision Questions and Answers (English and Kiswahili)

Free Kiswahili Notes, Exams, Schemes of Work, Lesson plans and other revision materials
Free Kiswahili Notes, Exams, Schemes of Work, Lesson plans and other revision materials

UFAHAMU:

Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali:

 

Mwangeka Mwachoni alizaliwa mwaka wa 1930 katika tarafa ya Mwanda, Wilaya ya Taita-Taveta. Angalikuwa hai leo bila shaka angalikuwa mmoja wa watu mashuhuri wenye kuheshimiwa kwa ujasiri wao.

Mwangeka alipata taabu mno utotoni wake kwa sababu ya malezi ya shida ya wazazi wake ambao walishindwa hata kumpeleka shule. Juu ya hivyo aliweza kuinuka na kuwa kijana mahiri sana tena mkakamavu na mchanga-mfu. Alikuwa akiwatii wazazi wake na kuwaenzi. Alijitwika jukumu la kuiangalia ile milki yao ndogo waliyokuwa nayo na kuwatumikia bila kinyongo. Ustadi aliokuwa nao Mwangeka umeweka kumbukumbu ya vitendo vya ushujaa wake wakati angali ni mdogo. Wakati huo, kila siku alikuwa akichunga ng’ombe wa baba yake milimani kulikokuwa na hatari za kila namna za wanyama wa mwitu. Siku moja alipowapeleka ng’ombe wao malishoni aliwaona simba wawili katika mlima Vuma waliotaka kuwashambulia wale ng’ombe. Mwangeka alipambana nao kwa uta na mshale na akaweza kuwaua. Hapo ndipo sifa zake za ujasiri ziliposambaa Taita nzima.

Mwangeka alikuwa mtu mwenye hekima na busara nyingi na alikuwa mwenye maarifa ya mambo mengi ya ajabu. Mojawapo ya mambo aliyoyajua ni vipi kajipinga na kujihami na shari za maadni wasiweze kumwona au kumjua alipo na hali yeye amewakabili na kuwatazama. Basi alipofika umri wa miaka ishirini na tano alianza kuwa mashuhuri na sifa zake zilizagaa kila mahali. Wakati huo alikuwa amekwisha oa. Alimwoa mwanamke aitwaye Magema, bibi ambaye mwanzo wa kuolewa alionyesha hubo nyingi kwa mumewe. Lakini baada ya miaka michache alianza kubadilika hulka na kuwa na umbeya na udadisi mwingi. Kila mara alikuwa akimsaili mumewe kuhusu ushujaa wake na mengi mengine yasiyostahili kuulizwa, bali mradi aelezwe tu. Alikuwa akistaajabu kumwona mumewe akiweza kuishi msituni kwa muda wa mwezi mzima bila chakula, na vile alivyoweza kwenda kwa miguu kutoka Kasigau mpaka Mwanda, mwendo wa kilomita mia mbili, bila kuchoka. Pia, ilikuwa ikistaajabisha vile alivyoweza kupotea asionekane na maadui zake (ambao wakati huo walikuwa ni wazungu) akiwacha nyuma kivuli chake ambacho ndicho kikiwashambulia na kuwaua maadui hao.

Siku moja bibi alimbembeleza sana mumewe amweleze maarifa na miujiza atumiayo, lakini Mwangeka alikataa kabisa kumdokezea habari hiyo. Mwishowe kero lilizidi na Mwangeka hakuweza tena kumkatalia.

Aliona heri amweleze lakini alimkanya asiweze zabizabina na kumweleza mtu yeyote, kwani hiyo ilikuwa siri yake. Akitoa siri hiyo kumwambia mtu, maisha yake yatakuwa hatarini, mahasimu zake wakikipiga kivuli chake.

Mwangeka alifanya kazi kubwa katika kuupigania uhuru wa Kenya. Aliwafukuza wazungu na kuwaua wengi. Huu ndio wakati ambapo Taita, na Kenya kwa jumla, ilipomtambua Mwangeka kuwa ni kiongozi asiye na kicho, aliyejitolea maisha yake yote kwa ajili ya nchi yake. Yeye ndiye aliyekianzisha chama cha vijana wa kitaita kilichopigania usawa wa wataita. Alitembelea sehemu nyingi za Kenya na akakutana na Jemadari Dedan Kimathi, mmoja wa viongozi wa Mau Mau, wapiganaji wa vita vya uhuru. Viongozi hao wawili walizungumza na kushauriana namna ya kupambana na taabu zilizo wakabili na wakaahidiana kwamba watakuwa wakitembeleana mara kwa mara.

Huku nyuma nyumbani kwa Mwangeka mambo hayakuwa mema kama alivyofikiria. Baada ya yeye kuondoka wazungu wawili walifika na kumbembeleza mkewe awaeleze jinsi Mwangeka alivyokuwa akifanya. Kwanza mkewe alikataa kuwaeleza lakini baada ya kupewa gunia moja la mchele na shilingi kumi pamoja na kuahidiwa mambo mema kadha siku za mbele, aliwaeleza siri zake zote!

Ilikuwa usiku, tarehe 23 Machi 1966, Mwangeka alipoonekana amelala juu ya jabali kubwa, maiti, kiwiliwili chake kiasi cha maili tatu hivi kutoka kivuli chake.

You did not find what you wanted? Worry not. Just search for more notes and other learning/teaching materials, below. Simply type in the box below and click on the search button.

[ivory-search id=”14715″ title=”Default Search Form”]

(a)  Kisa gani kilimfanya Mwangeka kusifiwa kwa ujasiri katika Taita?        (alama 2)

  • Eleza sifa moja ya ajabu ya Mwangeka ambayo ilikuwa ikiwakanganya maadui zake.

(alama 2)

(c)  Eleza mabadiliko ya tabia ya mke wa Mwangeka.                                   (alama 3)

(d) Eleza sifa za Mwangeka zisizopungua tano.                                             (alama 3)

(e)  Wale wazungu wawili walifanya nini hata Mwangeka mwishowe akauawa?(alama 2)

(f)  Mwangeka alipokufa alikuwa kijana au mzee? Toa sababu.                     (alama 2)

(g)  Eleza maana ya maneno yafuatayo kwa namna yalivyotumika katika taarifa.(alama 6)

(i)   Mahiri: _____________________________________________________

  • Bila kinyongo: _______________________________________________
  • Hulka: ______________________________________________________

(iv) Mahasimu: ___________________________________________________

(v)  Akijitwika jukumu: ____________________________________________

(vi) Akimsaili: ____________________________________________________

 

 

SEHEMU YA B:

MUHTASARI:

 

Mzee Kondoo:       Wenyeji wa kijiji cha maendeleo; mabibi na mabwana pokeeni salamu zangu na shukrani kwa kuhudhuria mkutano huu. mimi pamoja na wazee wenzangu tuliamua kwa kauli moja kuwaita nyote hapa ili kujadili maendeleo ya kijiji chetu. Jambo linalotukera sisi wazee ni kwamba hali ya kijiji chetu inazidi  kuzoroteka. Kijiji chetu kiliitwa maendeleo sisi wazazi wake tulipokuwa na rai ya kuleta maendeleo. Wake kwa waume tulijifunga vibwebwe na kwa kweli juhudi zetu zilitoa matunda mema. Sasa nguvu  zimeanza kutuishia; leo tupo, kesho tutakuwa hatupo. Ninyi ndio mtakaoshika usukani. Kama tunavyoona, mambo yakiendelea namna hii, watoto wenu wataishi maisha ya dhiki. Tungependa ninyi wenyewe mtueleze kwa nini kijiji maarufu cha maendeleo kinarudi nyuma badala ya kuendelea mbele. Kila anayetaka kutoa hoja zake atapewa fursa ya kufanya hivyo. Lakini kwanza mzee mwenzangu ana machache ya kusema.

 

Rojo:         Asante sana mzee Kondoo. Kwa upande wangu naona kwamba tumekuwa pweza kujipalia makaa na kwa mintaarafu hii, maendeleo ya kijiji chetu yakaanza kuzoroteka. Kwa ufupi, tunazaa watoto tusioweza kuwalea. Ni hivi majuzi tu tulipomkuta mtoto mmoja amezirai …

 

Jara:          Wee! Kaa chini. Usituletee aibu hapa. Sisi ni watu wa kuheshimiwa. Ufahamu kwamba hukupewa fursa ili uanze kuchambua nyumba za wengine. Mungu mwenyewe alitoa amri kwamba watu wazae mpaka waijaze dunia.

 

Jilo:     Mimi namwunga mkono Jara. Anayosema Rojo hayafai kuruhusiwa kuzungumzwa tena.

 

Mzee Kondoo: Hatukuwaita hapa mje mgombane. Rojo hajataja jina la mtu wala hajamaliza kutoa hoja zake. Endelea bwana Rojo.

 

Rojo:         Nashukuru Mzee Kondoo. Ndugu, mimi nitatoa ule ukweli. Humu kijijini mwetu mna watoto ambao  hawaendi shule. Kazi yao ni kuzurura kila mahali na kuokotaokota mali za watu. Hata huingia mashambani mwa watu wakaiba matunda, mihogo, mahindi na mazao mengine wakapeleka mijini kuuza. Mimi kitendo kama hiki nakilaani kwani ndicho kinachorudisha maendeleo ya kijiji chetu nyuma.

 

Uledi:        Hayo usemayo ni kweli. Juzi walikuja usiku mwenyewe siko wakavunja mlango wakafagia nyumba yangu fyu! Vitendo vya vijana hawa vinadhihirisha ukosefu wa malezi bora. Mabwana na mabibi, mimi sipingi uzazi lakini yule azaaye atambue jukumu lake la kuwalea vizuri watoto hao hata kama ni ishirini: awalishe, awavishe, awatibu wawapo  wagonjwa, awafunze tabia njema na kupelekwa shuleni ili wakuapo waweze kujimudu na kushirikiana nasi katika kuendeleza kijiji chetu.

 

Heri:          Mabibi na mabwana mtaniwia radhi kwa vile ambavyo sina mke wala watoto. Hata hivyo sitasita kutoa maoni yangu. Wasemayo wenzetu ni ya kuungwa mkono. Watoto wakosao malezi bora ndio hatari katika kijiji chetu. Wakazi wa kijiji hiki wamekuwa waoga hata hawawezi kujenga maduka wakaendesha biashara zao humu.

 

Rojo:         Mbali na uhalifu wa vijana wetu sisi watu wazima pia twafaa kulaumiwa. Kwanza tumeshindwa kutimiza wajibu wetu kwa ajili ya ulevi. Tumeshiriki ulevi hata kwamba hatudiriki makazini wala mwetu majumbani. Vipi tutadumisha nidhamu katika jamii zetu? Pia tusisahau kwamba ili kuwa na jamii ya kuimudu siku hizi hali ya maisha imepanda juu na tusipokuwa na busara yatatushinda.

 

Uledi:        Zaidi ya hayo inatupasa tuzingatie miradi mbalimbali itakayotuletea maendeleo …

 

 

 

 

 

Maswali:

 

  1. Kwa nini wazee walikereka kuona kijiji chao kikizoroteka? (maneno 15)(alama 3)

      NAKALA CHAFU

      NAKALA SAFI

 

  1. Wanakijiji cha maendeleo wamekuwa pweza kujipalia makaa kwa vipi? (maneno 50)

(alama 8)

      NAKALA CHAFU

      NAKALA SAFI

 

  1. Uledi ana wazo gani kuhusu mpango wa uzazi? (maneno 15).               (alama 2)

      NAKALA CHAFU

      NAKALA SAFI

 

  1. Eleza mambo yanayozorotesha kijiji cha maendeleo? (maneno 50).   (alama 7)

      NAKALA CHAFU

      NAKALA SAFI

 

  1. SEHEMU YA C:

      MATUMIZI YA LUGHA

 

(a)  Andika kwa kinyume:

(i)   Nje kulikuwa kweupe.                                                                        (alama 1)

(ii)  Mzizimo                                                                                              (alama 1)

 

(b) Eleza matumizi ya “po” katika sentensi hizi.

(i)   Mjomba aliniuliza “Je, sikukuambia kuwa akomeleapo mwenyeji nawe mgeni koma  papo?                                                                              (alama 2)

(ii)  Eleza matumizi ya “kwa” katika sentensi hii:

Mwanariadha alijikaza kisabuni tulipomshangilia kwa nguvu.           (alama 1)

 

(c) Akifisha sentensi zifuatazo:

(i)   lahaula sijui kama kazi hii itamalizika                                                 (alama 2)

(ii)  siku ya jumapili mwezi wa aprili mwaka huu tutaenda mombasa      (alama 1)

 

(d) Eleza maana ya misemo hii :

(i)   Kulia ngoa.                                                                                          (alama 2)

(ii)  Kuwa mjango.                                                                                     (alama 3)

 

(e)  Kamilisha methali hii:

(i) Atupaye tope _______________________________________________(alama 4)

(ii)  Cha mkufuu mwanafuu ha, na akila hu, _________________________(alama 5)

 

(f)  Tumia kivumishi kwenye vifungo kukamilisha sentensi:

(i)   Tuleteeni ng’ombe yeyote __________________________ (-dogo) (alama 1)

(ii)  Ngoma  _________________________, ndiyo iliyotakikana. (-le)   (alama 1)

 

 

 

 

(g)  Andika sentensi zifuatazo upya kulingana na maagizo uliyopewa:

  • Mti wa zambarau ni rahisi kukatwa ikiwa unatumia msumeno. (Anza: “Ni rahisi … )                                                                                       (alama 2)

(ii)  “Kuna chai?” Mtoto aliuliza.   Maliza na …. Chai)                             (alama 2)

(iii) Tabasamu yake ilipotea haraka alipoambiwa kuwa alipatikana na hatia ya kuwa mlevi na kukosa adabu.                (Anza Aliishiwa na ….)                                                                                                                                        (alama 2)

(h)  Geuza sentensi zifuatazo katika hali ya mazoea:

(i)   Mtoto unavyomlea ndivyo anavyokuwa.                                           (alama 2)

(ii)  Matunda yanayoiva ndiyo yanayotundwa.                                        (alama 2)

 

(i)   (a)  Mke wa mwanao utamwitaje?                                                            (alama 1)

(b)  Yohana na Selemani ni ndugu, pia wataitanaje?                                (alama 1)

(c)  Msichana ambaye hajavunja ungo huitwaje?                                      (alama 1)

 

(j)   Eleza muundo/mpangilio wa sentensi hii:

Amenikasirisha                                                                                          (alama 3)

 

(k)  Tumia maneno  haya katika  sentensi.

(a) Hapiki hapakui.                                                                                    (alama 2)

(b) Hana kazi hana bazi.

 

(l)   Tumia amba katika sentensi hii.

Mtoto anayelia amepigwa na mwizi vibaya sana.                                     (alama 1)

 

SEHEMU YA TATU

USHAIRI:

 

Soma shairi hili, kisha uyajibu maswali yanayofuata:

 

  1. 1. Dunia yanishangaza, kwa mikiki na myujiza,

Yajaa sana kuwaza, ama nitajiumiza,

Kwa maovu kuigiza, nimejigeuza pweza,

Mola naomba ya jaza, nanuia kuwa mwema.

 

  1. Utu uzima wangia, masoma namalizia,

Michezo yanizidia, rafiki wana udhia,

Sipati wala tulia, masomo sijafalia,

Mwenyewe najichukia, vitabu sijavishika.

 

  1. Siku nazo zayoyoma, kesho nitasema nini?

Nitanena sikusoma, nitamdanganya nani?

Wazazi pesa wachoma, kunipeleka shuleni,

Kwa kuwa nimebaini, heri nitie bidii.

 

  1. Mawi yamenizunguka, mungu wangu nibariki,

Kujiasa ninataka, nifanye yote ya haki,

Ningependa kuamka, utepetevu sitaki,

Nyuma sipendi kubaki, ningependa kufaulu.

 

  1. Marafiki naeleza, kuwa nimeshachapuka,

Habari nazieneza, wala msije kumaka,

Ukweli ninawajuza, horomo nimeondoka,

Uvivuni nimetoka, niondoeni kundini.

 

6    Panda nalipulizia, kwa wa hapa na wa kule,

Nadhani nimesikia, mkazo natia shule,

Ukunguni nasusia, nataka kusonga mbele,

Sitaki zenu kelele, nidhamu naifwatile.

 

  1. Leo nisipokazana, kesho nitakula nini?

Nitawakidhije wana? Nitakuwa mtu duni!

Riziki takuwa sina, nitaitwa mkunguni,

Moto najipaliani? Heri nijikuze sasa.

 

  1. Mtegemea cha ndugu, atakufa maskini,

Ama atakuwa pwagu, aishie kifungoni,

Kwa nini niote sugu, na kweli i hadharani,

Sitajitia shimoni, nitayapenda masomo.

 

  1. Baibai masahibu, msipende kunighasi,

Nitavisoma vitabu, mitihani niipasi,

Nigeuke mahabubu, na mtu aso muasi

Hayana ya wasiwasi, yenu nyingi hayawani.

 

  1. Jongoo nimemtupa, na mti wake pamoja,

Sitataka tapatapa, ninaitafuta tija,

Nyingi pigeni malapa, hatavishwa makoja,

Kuna siku itakuja, mtakuja kuhiliki!

 

Maswali:

(a)  Andika kichwa mwafaka kinachofaa kuelezea shairi hili.                        (alama 2)

(b) Hili ni shairi la aina gani? Toa sababu zako.                                             (alama 2)

(c) Marafiki wa mwandishi wana tabia gani?                                                (alama 4)

(d)      Ni nini dhamira ya mtunzi?                                                                 (alama 2)

(e) Andika ubeti wa sita kwa lugha nathari.                                                  (alama 5)

(f) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa katika shairi

(i)  Mikiki                          (ii)  Kuyoyoma                        (iii)  Mkunguni

(iv)  Panda                         (v)  Sugu

 

  1. 10. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali :

 

  1. Ukitazama dunia, umbo lake huarifu,

Kuwa imeandaliwa, wageni watukufu,

Tayari kuwapokea, na mambo sufufu,

Ndani yake yamejaa, viumbe kuwanadhifu.

 

 

 

  1. Umbile huonyesha, namna ilivyotimu,

Yangoja kukaribishwa, katika mastakimu,

Yenye kila tamasha, machungu na matamu,

Maisha yanapokwisha, huiacha inadumu.

 

  1. Ajae ardhi hii, kutoka katika mimba,

Mzizini au yai, au katika kitumba,

Milki hakinai, ya mali wala mashamba,

Mwisho wa uhai, kaburi lake jemamba.

 

  1. Halii choyo kaburi, mtu uzima ukisha,

La upana shubiri, urefu pima yatosha,

Wala hadai fahari, tena hujifaharisha,

Akiwa hai fikiri, anavyopenda tamasha.

 

  1. Yalipo maziara, masikani ya maiti,

Huonyesha ishara, na pengine tofauti,

Dhaifu na bora, hawagombi hawateti,

Wazima kila mara, Pato linawasalitia.

 

  1. Mtu hashibi pato, hili huonyesha nini?

Laonyesha kama pito, kuwa yumo safarini,

Enda kuitika wito, bora usio kifani,

Ambao kila mtoto, wa Adam hutamani.

 

  1. Yumo katika safari, kila mwanadamu,

Haraka au usiri, kwenda imelazimu,

Epusha roho kahari, yake na Jahanamu,

Iwe katika fahari, mwili ukiwa kuzimu.

 

Maswali:

 

(a)  Pendekeza kichwa cha shairi hili.                                                             (alama 2)

(b) Mshairi amevitaja vitu aina ngapi vyenye uhai? Vitaje.                            (alama 4)

(c) Andika ubeti wa tatu kwa lugha nathari.                                                  (alama 5)

(d)      Eleza vina na mizani katika shairi hili.                                                            (alama 3)

(e) Eleza ujumbe wa mshororo:

“Halii choyo kaburi, mtu uzima ukishe.”                                                   (alama 2)

(f) Onyesha vile uhuru wa kishairi ulivyotumiwa.                                         (alama 4)

 

KISWAHILI I

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA INSHA:

 

  1. Kila insha ina alama 20 – jumla 40.
  2. Tumia mtindo ufuatao kwa kusahihisha.

Maudhui –       5

Mtindo            –           4                      Tahajia  –   3

Sarufi –           6

Msamiati –       5

20

 

MAUDHUI:

Kadiria maelezo anayotoa mwanafunzi kuhusu anwani. Angalia ikiwa ametaja hoja mwafaka na ikiwa amejibu swali; je:

1)   Ametaja mada/hoja zote? –     5

2)   Ametaja nusu?                        –           2 ½

3)   Ametaja chini ya nusu?           –           2

4)   Hakutaja chochote      –           0

 

Mtahini ana uhuru wa kukadiria alama kama atakavyoongozwa na majibu kutoka kwa mwanafunzi.

 

MTINDO:

Ni mpangilio wa insha – utangulizi, maelezo na mwisho. Ni mtiririko wa mawazo na namna mwanafunzi anavyowasilisha mawazo yake. Mtahini akadirie kulingana na jibu.

 

SARUFI:

Ni makosa ya sarufi ya lugha ya Kiswahili. Kila kosa litokeapo, alama (.5) huondolewa ambayo ni nusu alama. Kossa likirudiwa haliadhibiwi mara mbili. Usiondoe zaidi ya alama 6  yaani nusu 12.

 

MSAMATI:

Ni uafaka wa matumizi ya misamiati ya lugha. Ni uzito wa lugha ya mwanafunzi. Mtahini akadirie.

 

HIJAI:

Ni makosa ya uendelezaji ambayo huondolewa kutoka jumla ya alama aliyopata mwanafunzi. Usiondoe zaidi ya alama 3 yaani nusu 6.

 

MASWALI

 

1.(a) Mahindi

– Aeleze ni aina gani ya mimea, faida yake au matumizi yake kwa binadamu.

– Aeleze namna shamba linavyotakikana kutayarishwa halafu namna ya kupanda- kuongezea mbolea n.k.

– Utunzaji  wa mahindi inapokuwa shambani hadi uvunaji – mitindo ya uvunaji.

 

(b)  Nyanya – Mtindo ni huo wa hapo juu.

2,3,4 – Mtahini atasahihisha kulingana na majibu ya mwanafunzi maana majibu ni mbalimbali kulingana na chaguo la mwanafunzi.

 

SEHEMU YA PILI

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

UFAHAMU, UFUPISHO, MATUMIZI YA LUGHA

 

Jinsi ya kutuza na kuadhibu makosa:

Ufahamu:  (Muhtasari na matumizi ya lugha

Ondoa alama ½ kwa kila kosa  la sarufi. Usiondoe zaidi ya nusu ya alama zote katika swali.

  • Ondoa alama ½ kwa kila kosa la hijai, usiondoe zaidi ya nusu sita yaani alama tatu katika swali zima.

 

Kuadhibu makosa:

  • Sarufi – adhibu makosa kumi na mbili ya sarufi. Kila kosa alama ½ 12 x ½ = 6.

 

  • – Tahajia – adhibu makosa kumi ya hijai, kila kosa alama ½ 10 x ½ = 5.

–  Makosa ya hijai yanagusia mwendelezo kama paba badala ya baba.

–  Kuunganisha mchezafibora – mchezaji bora.

–  Kutenganisha – mwana sheria badala ya mwanasheria.

 

  • Mtiririko – pima alivyotiririsha hoja zake. Je, ni wastani? 1 ½ ju ya wastani ; 2 ½ au chini ya wastani (1). Usimpe sifuri (0) katika mtiririko.

 

  • Ikiwa mtahiniwa hakuelezea hoja kikamilifu, mpe nusu alama ya ile yote.

 

Mwongozo wa kusahihisha ufahamu:

 

  • Jinsi alivyoweza kupambana na simba wawili waliotaka kuwashambulia ng’ombe wao katika mlima wa vuma na kuwaua.

      (Maelezo kamili  –  alama 2)

 

(b)  Sifa yake ya kuweza kujihami na kukikinga asionekane na maadui zake au kujulikana

alikokuwa ilhali yeye angewakabili na kuwatazama.                               (alama 2)

 

(c)  –   Mbeleni alimpenda Mwangeka sana lakini baadaye tabia yake ikabadilika akaanza

kuwa   na umbeya huku akidadisi mumewe apate kujua mengi kumhusu.

  • Alibadilika na kumsaliti mumewe kwa kutoboa siri kwa wazungu waliomwua Mwangeka, kwa hivyo alibadilika kutoka ile tabia yake ya kuaminiwa na mumewe kuwa mwaminifu na kuwa msaliti.                         (alama 5)

 

(d) Sifa za Mwangeka:

  • Mtiifu kwa wazazi.
  • Asiye na kingongo atendapo mema.
  • Mwenye hekima na busara.
  • Mwenye maarifa ya mambo mengi.
  • Kiongozi shupavu. (alama ½ x 6  =  3)

 

(e)  Walimwendea mkewe Mwangeka na kumwuliza jinsi mumewe alivyokuwa akifanya. Alipojizuia kutoboa siri alihongwa kwa gunia moja la mchele na shilingi kumi na kuahidiwa mema siku za baadaye naye akaeleza siri ambayo ilisaidia kuuwawa kwa mumewe (Mwangeka).                                                  (alama 2).

 

 

 

(f)  Kijana kwa sababu alikuwa na miaka 36. Kwa hivyo mtu wa makamo mwenye

nguvu.                                                                                           (alama 2)

 

(g)  (i)   Mahiri – mwenye ujuzi na hodari kufanya mambo, mwenye busara.

  • Bila kinyongo – bila chuki au uchungu.
  • Hulka – mwenendo au tabia.
  • Mahasimu – maadui.
  • Alikitwika – alifanya wajibu huo bila kulazimishwa.
  • Akimsaili – Akimdadisi, akimhoji, akimwuliza – uliza maswali kwa minajili. (alama 6)

Mwongozo wa kusahihisha muhtasari:

  1. – Kilikuwa kikiongoza katika maendeleo.

–     Kulikuwa na hali ya kuzorota.

–     Hali hiyo ingeleta dhiki baadaye.                                           (alama 1×3 = 3)

 

  1. (1) Kuwa walevi.
  • Kuzaa watoto wasioweza kuwalea.
  • Hawafanyi kazi.
  • Hawawafunzi watoto tabia nzuri, wanawaletea madhara. (alama 4×2 = 8)

 

  1. Uzazi ni mzuri lakini wazazi wazingatie wajibu wao. (alama 2)

 

  1. kutopanga uzazi:
  • Hawafanyi kazi.
  • Hawawalei watoto wao vizuri.
  • Wao walewa.

(3 x 2 = 6 – alama moja kwa maelezo = 7)

 

Mwongozo wa kusahihisha: Matumizi ya lugha:

 

(a)  (i)   Ndani kulikuwa kweusi.                                                                     (alama 1)

(ii)  Mzizimo – ari au fukuto.                                                                     (alama 1)

 

(b)  (i)   Po – wakati.                                                                                         (alama 1)

(ii)  po – mahali.                                                                                         (alama 1)

 

(c)  (i)   Lahaula! Sijui kama kazi hii itamalizika?                                (alama 2    ½ x 4)

(ii)  Siku ya Jumapili mwezi wa Aprili mwaka huu tutaenda Mombasa.

( ½ x 4 alama 2)

(d) (i)   Kulia ngoa – kuhusudu.                                                                       (alama 2)

(ii)  Kuwa mjango – kuwa kazi bure                                                          (alama 2)

 

(e)  Kamilisha methali hii:

(i)   Atupaye tope hujichafua naye.                                                           (alama 2)

(ii)  Cha mkufuu mwanafuu ha, na akila hu, cha mwanafuu mkufuu hu akila ha.

(alama 2)

(f)  (i)   Mdogo.                                                                                               (alama 1)

(ii)  Ile.                                                                                                       (alama 1)

 

 

(g)  (i)   Ni rahisi kuukata mti wa zambarau ukitumia msumeno.                    (alama 2)

(ii)  Mtoto aliuliza kama kulikuweko na chai.                                           (alama 2)

 

(iii)Aliishiwa na tabasamu haraka alipoambiwa kuwa alipatikana na hatia ya kuwa mlevi na kukosa adabu.                                                    (alama 2)

 

(h)  (i)   Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.                                                      (alama 2)

(ii)  Matunda yaivayo ndiyo yatundwayo.                                                            (alama 2)

 

(i)   (a)  Mkaza mwana.

  • Kigoli/kigori.

 

(j)   A   –     kiambishi ; kiwakilishi; kiima (yeye_)

me –     kiambishi ; kiwakilishi cha wakati (wakati timilifu).

ni   –     kiambishi ; kiwakilishi ; kitendewa ; (mimi)

kasir –  suna la kitenzi.

Insha – kielezi cha jinsi (jinsi ya kufanya)

( ½ x 5 = 2 ½ )  +  ( ½ ya maelezo)

 

(k)  (a)  Mvivu mfano itapiki mzurura tu.                                                        (alama 2)

(b)  Hana chochote.                                                                                   (alama 2)

 

(l)   Mtoto ambaye analia amepigwa na mwizi vibaya sana.                           (alama 1)

 

SEHEMU YA TATU

USHAIRI MWONGOZO

 

  1. USHAIRI:

(a)  – Kujiasa na makanyo.             –   Zinduko.                 –   Kujitoa uvivuni.

–    Buriani n.k.

      (yoyote mwafaka alama 2)

 

(b)  (i)   Tarbia – lina mistari minne katika kila ubeti.

(ii)  Ukaraguni – kila ubeti una kina chenye silabi tofauti na ubeti mwingine

kinyume na ukara wa mtiririko                                                                                                                      (kutaja alama 1  ;  kutoa sababu alama 1  ; alama 2)

 

(c)  Tabia ya uvivu:

  • Uzururaji –    Utovu wa nidhamu.
  • Kutozingatia maisha ya baadaye. (alama 4×1 = 4)

(d)

  • Kuzindua mtu anayepotoka.
  • Kumuasa mtovu wa nidhamu.
  • Kumshauri yeyote anayeshiriki katika utovu wa nidhamu n.k.

(hoja moja 1×2 = 2)

 

(e)  Nawatangazieni nyote popote mlipo kuwa natumai mmepata habari kuwa mimi sasa bidii yangu iko shuleni. Nimeamua kuongoka kinidhamu.       (alama 5)

 

(f)  (i)   Mikiki – shuguli za kinguvunguvu.

  • Kuyoyoma – kupotea kwa haraka, kutokomea, enda bila kutazama.
  • Mkunguni – mvivu, mlegevu, goigoi.
  • Panda – tarumbeta, baragumu, parapanda.
  • Sugu – jeuri, mwenye kichwa kikubwa, asiyejali, asiyesikia maonyo kabisa.

(jumla alama 5)

 

  1. (a) – Maisha ya mwanadamu duniani.
  • Hatima ya maisha ya mwanadamu ni kifo.

(hoja yoyote sawa – alama 2)

 

(b) Aina tatu:

  • Wanaozaliwa – kutoka mimbani. –     Mimea – kutoka mzizi.
  • Ndege na wadudu – kutoka kwenye yai au mfuko.

 

(c)  Viumbe vyote vijazavyo dunia ikiwa ni wa kuzaliwa, mimea. Kutoka kwenye yai au mfuko hawezi kutosheka na mali akiwa hai lakini mwishowe hungia kaburini ambayo huchukua sehemu ndogo ya ardhi.

 

  • – Vina vinabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.

–   Vina vya kati na mwisho ni tofauti katika kila ubeti.

–   Mizani hailingani katika mishororo ya kila ubeti ; mfano ubeti wa kwanza:

mshororo wa kwanza una mizani 16

na mishororo wa pili una mizani 15

                  (hoja 3×1 =  3)

 

(e)  Maana ni kuwa kaburi i tayari kila wakati kupokea wafu na hivyo kila mwanadamu awe tajiri au maskini ajue bayana kuwa siku moja ataaga dunia na kuyaacha au kuacha mali yake yote.

 

(f)  Uhuru wa kishairi:

(i)   Inkisari – kufupisha maneno.

Mfano:      jemamba  –  jembamba

Yangoja  –  yanangoja.

(ii)  Mazda – kurefusha maneno

Mfano:      Linawasalitia  –  linawasaliti.

(kutaja alama 1 kwa kila mfano kutoa mifano miwili moja kwa kila moja –

alama 2  –  2×2 = 4)

 

KISWAHILI II

SEHEMU YA KWANZA

Insha

 

Insha zote zizipungue maneno 400 kila moja. Kila insha ina alama 20.

 

  1. Andika insha ya mazungumzo ya simu kati ya Kirubi na Ojilo.
  2. Safari ni hatua.
  3. Tatizo la vijana wanaorandaranda mijini haliwezi kutatuliwa. Jadili
  4. Namna ya kupika Ugali.

 

 

KISWAHILI YA PILI

UFAHAMU, UFUPISHO, MATUMIZI YA LUGHA

 

Sehemu ya kwanza – UFAHAMU

 

Nchi zetu za Afrika zinakumbwa sana na ukosefu wa mvua. Inasemekana ya kwamba jangwa linazidi kutanda katika bara hili, kwa hivyo ni wajibu wetu kujiandaa na kuchukua hatua kadha wa kadha ili tuweze kupambana na ukavu huu, kwani wahenga walisema, “Uwahi udongo uli maji.”

 

Kwa hakika ukavu huu unasambaa katika bara hili na unatutia hofu kubwa. Imekuwa sana tunategemea nchi za kigeni kutusaidia. Tukichunguza zaidi sababu kubwa ya ukosefu wa mvua ya kutosha ni ukataji wa miti. Kwa hivyo tuhakikishe kuwa tutapanda miti kwa wingi wakati wa mvua. Serikali ya Kenya inahimiza sana upandaji wa miti katika sehemu mbalimbali za nchi. Pia lazima tuhakikishe kwamba baada ya mche kupandwa, kufanywe mipango na kupatikane watu ambao wataiangalia na kuipalilia hadi itakapokuwa mkubwa. Ni wazi kwamba tumetilia mkazo wa kupanda miche lakini hatujazingatia miche hii kuangaliwa kwa kunyunyiziwa maji wakati wa ukame.

 

Hatua ya kuchimba visima, katika sehemu zenye ukavu ni jambo la muhimu sana, kwani maji ya visima yataweza kutumika majumbani na pia kunyunyizia mimea. Maji kwa binadamu ni kitu muhimu sana kwa sababu bila ya maji hakuna uhai. Huko Australia, visima vingi vimechimbwa katika sehemu zenye ukame kwa minajili ya kuwapatia wakazi wa sehemu hizo maji ya nyumbani, mifugo na kunyunyizia mimea.

 

Maji ya mvua na yale yanayochuruzika mitaroni, hukusanywa na kutumiwa kwa kunyunyizia mimea. Mashamba yanayonyunyuziwa maji ya aina hii, hunawiri na kustawi sana. Maji ya mito ambayo huchuruzika baharini, lazima tuyatumie baada ya kuiondoa chumvi ndani yake. Vile vile, tujaribu tuwezavyo kupanda mimea ambayo itatupa chakula cha kutosha ili tuweze kujitegemea badala ya kuzitegemea nchi za kigeni.

 

(a)   Mwandishi ametumia methali “uwahi udongo uli maji” akimaanisha nini hasa? (alama 3)

(b)  “Haitoshi tu kupanda miche na kutulia”. Kulingana na yaliyomo katika taarifa hii, ni hatua gani               zingine zinazohitajika ili kufaulu katika mradi huo wa upanzi?                                    (alama 3)

(c) Taja jitihada zozote mbili zinazochukuliwa na serikali ili kukabiliana na shida ya

ukosefu wa  mvua / maji(alama 4)

(d)     Kwa nini maji ya baharini hayatumiwi moja kwa moja?                               (alama 2)

(e)     Kwa nini nchi nyingi za bara la Afrika zinategemea nchi za kigeni?             (alama 3)

(f)      Maneno yafuatayo yametumiwa kuleta maana gani?                                   (alama 5)

(i)      Kutanda____________________________________________________

(ii)     Miche_____________________________________________________

(iii)    Kunyunyizia_________________________________________________

(iv)    Hunawiri__________________________________________________

(v)     Kustawi___________________________________________________

 

 

 

 

 

 Muhtasari

 

Hapo kale mfanyi-biashara mmoja alisafiri akenda kufanya biashara katika nchi ya mbali na kwao. Baada ya kuuza bidhaa zake alifunga safari ya kurudi kwao. Alisafiri msitu na nyika hata akafika kwenye jangwa. Ilimbidi alivuke hilo jangwa.

 

Mfanyi biashara huyo alisafiri siku kadha jangwani. Siku hizo za kale kulikuwa hakuna magari. Mfanyi-biashara alikuwa amepanda farasi. Baada ya siku chache farasi alichoka sana akaanguka na kufa. Mfanyi-biashara sasa ikambidi asafiri kwa miguu.

 

Hatimaye maji aliyokuwa nayo yalikwisha yote, akawa hana hata tone la maji ya kunywa. Kiu ilimbana lakini maji yalikuwa hayapatikani jangwani kote. Ilimpasa aanze kusafiri usiku usiku, kwa sababu mchana jua lilikuwa kali sana na angalisafiri wakati huo kiu ingalimzidi.

 

Baada ya kusafiri siku mbili tatu katika hali hii, alijiona hawezi tena kuendelea. Alikuwa yu hoi, alishindwa hata kunyanyua mguu. Kwa bahati siku ile alipita msafiri mwingine amepanda ngamia. Alipomwona mfanyi biashara katika hali ile alisimama na kumwangalia. Mfanyi-biashara alimwomba yule msafiri maji.

See also  Biology notes form 1-4; Free KCSE downloads

 

Msafiri alimjibu, “Maji niliyonayo ni kiasi ya kunitosha mimi tu, siwezi kukupa.”

 

Mfanyi-biashara alisema, “Mimi ni tajiri sana. Milki yangu haihesabiki. Huko kwetu nina majumba na mashamba mengi. Mimi ni tajiri nikukabidhi mali hiyo yote nawe unipe hicho kiriba chako cha maji.”

 

Msafiri alimjibu, “Mimi sina haja ya mali iliyoko nchini kwenu mali hiyo sitaweza kuitumia nchini kwetu.”

 

Mfanyi-biashara aliwaza kisha akamwambia, “Hivi hapa nina kifuko kimejaa almasi na lulu. Hizi nilizinunua huko nilikotoka. Biashara ilinipatia faida nyingi sana. Je, utachukua almasi na lulu hizo zote, nawe unipe kiriba cha maji?”

 

Msafiri alikubali. Mfanyi-biashara alipata maji akanywa na kukata kiu yake. Maisha yake yakaokoka na kuepukana.

 

Maswali

 

(a)   Eleza matatizo yaliyomkabili mfanyi-biashara katika safari yake toka mwanzo hadi

mwisho wa safari. (Maneno 30 – 40)                                                                (alama 8)

Nakala chafu

      Nakala safi

 

(b)   Katika kila janga mfanyi-biashara alipita, kulijitokeza suluhu. Eleza jinsi hali hii

inavyosawirika.

(Maneno 20 – 30)                                                                                           (alama 6)

      Nakala chafu

      Nakala safi

 

 

(c)  Eleza kwa ufupi mambo muhimu yanayojitokeza katika mazungumzo baina ya msafiri na mfanyi-biashara. (Maneno 40)  (alama 6)

      Nakala chafu

      Nakala safi

 

Matumizi ya Lugha

 

(a)     Andika sentensi ifuatayo bila kutumia “amba”

(i)      Jitu ambalo linatusumbua sharti liadhibiwe vikali.                               (alama 1)

(ii)     Weka sentensi ifuatayo katika hali ya mazoea. Mmea ambao unapandwa

katika msimu wa masika unamea.                                                        (alama 2)

 

(b)     Badilisha sentensi hizi hadi usemi wa taarifa

(i)      “Nitarudi tu ikiwa mtakubali kuomba msamaha.” Juma alisema.  (alama 2)

(ii)     “Elezeni vile mlivyokuja hapa na namna mtakavyokwenda.” Mwalimu mkuu

alisema                                                                                        (alama 3)

 

(c)     Fuata maagizo uliyopewa baada ya kila sentensi ili kujibu maswali haya.

(i)      Aliogopa kumwangalia simba aliyekula mzoga. (Tumia neno ‘Ogofya’ bila

ya kubadilisha maana ya sentensi)                                                (alama 2)

(ii)     Mti wa zambarau ni rahisi kukatwa ukiwa unatumia msumeno. (Anza Ni

rahisi . . .)                                                                                     (alama 2)

 

  1. d) (i) Eleza maana na matumizi ya methali hii                                      (alama 2)

Kila mchukuzi husifu mzigo wake

(ii)     Kamilisha tashbihi hizi                                                                 (alama 2)

……………kama mauti

Nuka kama…………..

 

(e) (i) Kanusha sentensi hii                                                                             (alama 2)
           Tungewalaki kama tungejua watakuja
(ii)  Sahihisha sentensi ifuatayo na uiweke katika wingi                           (alama 2)
Ningalifanya kazi ningekuwa tajiri

(f)  Tunga sentensi nne kuonyesha matumizi na maana nne za kijineno ki

(g)     Tumia kivumishi kilichoko kwenye mabano kukamilisha sentensi      (alama 4)

(i)      Bibi yule alinunua gari _______________ (-pya)

(ii)     Mwizi alifukuzwa na mbwa _______________ (-angu)

(iii)    Mti (-ingine) _________________ uliangushwa badala ya ule wa kwanza.

(iv)    Nyoka aliingia ______________ (-le) shimoni.

 

(h)     Unda majina mawili kutoka vitenzi hivi na utumie katika sentensi ili kubainisha

maana                                                                                                (alama 4)

(i)      Safiri

(ii)     Zaa

 

(i)      Akifisha kifungu hiki

Yohana na emanueli walifunga safari wakielekea mashariki kusini na hatimaye

magharibi walifika huko novemba mwaka jana walipokuwa wakirudi walimkuta

mwalimu mkuu njiani ambaye alishtuka kuwaona pale                                                 (alama 4)

(j)      (i)      Geuza sentensi hii hadi udogo                                                     (alama 2)

Nyoka yule mrefu alifukuzwa na watu wengi.

(ii)     Eleza umuhimu wa sehemu hizi za mwili

*       Figo

*       Moyo

 

SEHEMU YA TATU

USHAIRI

 

  1. Soma mashairi yafuatayo kisha ujibu maswali

Cheo cha mtu hupanda, ukipata mke mwema,

Kula chachu na maganda, mfano kama mnyama,

Na nyumba iwe kibanda, si nzuri ya kutazama,

Utaona umewanda, moyo umekuterema.

 

Mke mwema ni johari, yenye furaha daima,

Awe hasa na saburi, na adili na huruma,

Hata ukiwa fakiri, hutimizi pato jema,

Utaona tajiri, maliki dunia nzima.

 

Mke akiwa mbishi, wa kushindana kusema,

Na majivuno na mashi, na ulimi wake pima,

Hata kama wala pishi, wali na kilo ya nyama,

Utajiona waishi, duniani huna kima.

 

Mke mrembo si hoja, hili nimekwisha pima,

Nimepima rejareja, kila jambo kutazama,

Kujumlisha pamoja, mambo yalivyosimama,

Nikaona kuwa tija, ndogo kuliko gharama.

 

Awe mwema mke wangu, nani hapendi kusema?

Wema asili ya ungu, milele una heshima,

Kuwa wema walimwengu, ni wajibu na lazima,

Wema dawa ya machungu, moyoni yanayouma.

 

Maswali

 

(a)     Kulingana na shairi hili, mke mwema ana faida gani kwa mumewe?            (alama 3)

(b)     Mke mwema ana sifa gani?                                                                            (alama 3)

(c)     Mwandishi wa shairi hili alikuwa na dhamira gani katika kutunga shairi hili? (alama 3)

(d)     Eleza kwa ufupi muundo wa shairi hili.                                                         (alama 6)

(e)     Maneno yafuatayo yametumiwa katika shairi kuleta maana gani?                (alama 5)

(i)      Chachu

(ii)     Johari

(iii)    Saburi

(iv)    Mbishi

  • Pishi

 

 

 

  1. Nataka nikupe chanzo, weka katika moyo,

Kishike kwa mkazo, hata kizae mazao,

Ukifanya bidiizo, kushawishi utakayo,

Utaona mfulizo, kwako yanakuja mbio

 

Husemwa Alexander, shujaa Macedonia,

Ambaye alishinda, karibu nzima dunia,

Alipokosa pa kwenda, tena kushambulia,

Kwa huzuni alikonda, akadiriki kulia,

 

Ingawa vita vigumu, yeye alivipenda,

Kwa moyo aliazimu, daima mbele kwenda,

Moyo kuitia hamu, mashaka kuyashinda,

Ndilo linalolazimu, kila mtu kutenda.

 

Moyo ukiulegeza, kila kitu kigumu,

Utaishi na kuoza, hupati kuonja tamu,

Lakini ukijikaza, ipasavyo mwanadamu,

Katika mwangaza, utakuwa na sehemu.

 

Moyo kuupa mwanzo, wa kushindwa hustawi,

Utaona mzozo, unalotaka haliwi,

Na hili ni katizo, ya faida ya uhai,

Peponi halina tuzo, na hapa ni uadui

 

Hili linahasiri, moyoni kulidhibiti,

Mabaya ukifikiri, yaliyo mema hupati,

Na kila wazo la heri, hukaribisha bahati,

Fikira iliyo nzuri, sawasawa na yakuti.

 

Maswali

(a)     Kilichomfanya Alexander kufaulu katika kadhia zake ni nini hasa?             (alama 3)

(b)     Andika ubeti wa nne katika lugha ya nathari.                                               (alama 4)

(c)     Kuna athari gani kwa kukosa moyo wa ujasiri?                                             (alama 3)

(d)     Mtunzi huyu ana dosari gani kwa upande wa muundo wa shairi?                (alama 4)

(e)     ‘Kwa huzuni alikonda, akadiriki kulia.’ Ni kwa nini ilitukia hivi?                (alama 3)

(f)      Eleza maana ya maneno haya.                                                                       (alama 3)

(i)      Akadiriki

(ii)     Kushawishi

  • Kulidhibiti

 

KISWAHILI II

Mwongozo wa Kusahihisha

SEHEMU YA KWANZA  Insha

 

Maudhui – 5

Mtindo – 4

Msamiati – 5

Sarufi – 6

Hijai – aondolewe alama zisizozidi 3

*        Ukadiriaji wa alama hizo ni jukumu la mwalimu kwa kutegemea kazi ya

mwanafunzi.

–        Maudhui

*        Yaweza kuhusu mada yoyote.

*        Mwanafunzi aweza kuonyesha lengo au kiini cha mazungumzo

*        Aonyeshe mawazo kadha wa kadha yanayohusu kiini cha mazungumzo

–        Mtindo

*        Atenganishe jina na maneno yake hasa aghalabu kwa kutumia koloni.

*        Atumie lugha ya simu – kama vile ‘Hallo’ n.k.

*        Atangulize mazungumzo yake kwa maamkuzi, kujitambulisha na kutaja lengo la

kupiga simu.

*        Aendeleze mazungumzo yake ipasavyo.

*        Aitimize kazi yake na ikiwezekana amalizie maagano.

–        Msamiati

*        Atumie lugha na sajili mwafaka.

–        Sarufi

*        Kila kosa la sarufi linapojitokeza, liadhibiwe na linaporudiwa, lionyeshwe tu.

*        Atangulize kazi yake kwa kueleza maana ya methali na matumizi, au atoe kisa

moja  kwa   moja.

*        Kisa kiweze kuthibitisha ukweli wa methali hii

*        Aitimize kazi yake

(ii)     Swali la TATU

*        Aonyeshe pande zote za swali.

(iii).   Swali la NNE

*        Atumie lugha ya maelezo na aonyeshe hatua kwa hatua.


SEHEMU YA PILI

UFAHAMU, UFUPISHO, MATUMIZI YA LUGHA

Mwongozo wa Kusahihisha .

 

(a)     Kupambana na tatizo la kutanda kwa jangwa barani kabla halijapita kimo au

kuchukua hatua za tahadhari mapema ili kuzuia jangwa kama kungali

kunawezekana.                                                                                    (alama 3)

 

(b)     *        Kuangalia miche / kutunza

*        Kupalilia

*        Kunyunyiziwa maji wakati wa ukame                                   (hoja tatu 3×1 = 3)

 

(c)     *        Serikali ya Kenya inahimiza upandaji miche.

*        Australia imechimba visima katika sehemu zenye ukame.                    (2×2 = 4)

 

(d)     Yana chumvi ndani yake.                                                                              (alama 2)

 

(e)     *        Hawapandi mimea inayowapa vyakula

*       Ukavu / ukame ambao unasambaa

                    (2 x 11/2 = 3)

 

 

 

 

(f)      Kutanda – kuenea

Miche – Chipukizi, mimea inapoanza kutoa majani yake juu ya ardhi

Kunyunyizia – kumwagia maji

Hunawiri – Hung’aa / kufanya vizuri / vyema / kupendeza

Kustawi – Kukomaa

 

Muhtasari

 

(a)     *        Kusafiri msituni

*        Kupitia jangwa

*        Hakukuwa na magari

*        Farasi kuchoka na kufa / kukosa namna ya kusafiria

*        Maji aliyokuwa nayo kwisha

*        Kiu kumbana

*        Kusafiri usiku, giza

*        Kuwa hoi / mahtuti

*        Kukatazwa maji na msafiri                                           (hoja ozote tatu 6×1 = 6)

 

(b)     *        Kukosa gari – kupata farasi

*        Jua kali ya jangwa – kutembea usiku

*        Kiu – Kutembea usiku / kupata mtu wa kumpa maji

*        Msafiri kukataa mali ya mfanyi-biashara – kutoa lulu na almasi.   (4 x 11/2 = 6)

 

(c)     *        Mfanyi-biashara kuomba maji msafiri kwa kumuahidi mali

*        Msafiri kukataa mali ya mfanyikazi na kutoona thamani yake

*        Msafiri kumkataza mfanyi-biashara maji

*        Mfanyi-biashara kumuonyesha lulu na almasi msafiri

*        Msafiri kukubali kumpa maji mfanyi-biashara

                    (hoja ozote tatu 6×1 = 6)

a        –        6

b        –        6

c        –       5

Utiririko –   3

Jumla         20

 

Matumizi ya lugha

 

(a)(i)  Jitu linalotusumbua sharti liadhibiwe vikali

(ii) Mmea upandwao / ambao hupandwa katika msimu wa masika humea.(Alama 2)

 

(b)(i) Juma alisema ya kuwa / kuwa / ya kwamba / kwamba angerudi tu ikiwa / kama             

wangekubali kuomba msamaha.                                                                  (Alama 2)

(ii) Mwalimu Mkuu aliwataka / aliwaambia waeleze vile walivyoenda hapo na namna wangeenda / watakavyoenda.                                                                                            (Alama 3)

 

  1. c) (i)      Simba aliyekula mzoga alimuogofya kwa hivyo hakumwangalia       (Alama 2)

(ii)     Ni rahisi kukata mti wa zambarau ikiwa unatumia msumeno             (Alama 2)

 

 

 

(d)     (i)      Mtu mwenye shida ndiye ajuaye shida hizo. Kila mtu ana matatizo na hakuna

haja                                                                        ya kuwaeleza wengine.            (Alama 2)

(ii)     Hakika kama mauti.                                                                             (Alama 2)

 

(e)     (i)      Hatungewalaki kama hatungejua hawaji                                             (Alama 2)

(ii)     Tungalifanya kazi tungalikuwa matajiri au Tungefanya kazi tungekuwa tajiri. (Alama 2)

 

(f)      *        Ki ya Masharti

*        Ki ya udogo

*        Ki ya kukanusha

*        Ki ya lugha kwa mfano Kikamba

*        Ki ya ngeli ya KI-VI

*        Ki ya jinsi / namna kwa mfano tembea kijeshi na kadhalika                 (4×1 = 4)

 

(g)     (i)      Jipya

(ii)     Wangu

(iii)    Mwingine

(iv)    Mle                                                                                                        (4×1 = 4)

 

(h)     (i)      Safari / msafara / usafiri

(ii)     Mzazi / Mzaliwa / Uzazi                                                                      (2×2 = 4)

 

(i)      Yohana na Emanueli walifunga safari wakielekea Mashariki, Kusini na hatimaye Magharibi. Walifika huko Novemba mwaka jana. Walipokuwa wakirudi, walimkuta Mwalimu Mkuu njiani ambaye alishtuka kuwaona pale.

(Sehemu 12 = 12 x 1/3 = 4)

 

(j)      (i)      Kijoka kile kirefu kilifukuzwa na vijitu vingi.                                   (Alama 2)

(ii)     Figo – husafisha damu

Moyo – husambaza damu mwilini                                                         (2×1 = 2)

 

  1. Uvivu

*        Kulaza damu kwa Ame na zidi kumewaletea umaskini

*       Mwalimu anapolala darasani anasababisha elimu duni ambayo hatimaye                         inakuwa umaskini maana wanafunzi hawanufaishwi na elimu.

*        Utegemeaji wa misaada unaleta umaskini.

         

SEHEMU YA TATU

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

Ushairi

 

9.(a)  *        Mtu hupanda cheo

*        Mtu huwanda hata ingawa anakula maganda

*        Moyo unamterema                                                                     (Hoja 3 x 1 = 3)

 

(b)     *        Ni johari

*        Ana furaha daima

*        Sana subira

*        Mwadilifu                                                                                   (Hoja 3 x1 = 3)

 

(c)     *        Kutoa mawaidha kwa wanawake wawe wema

*        Kundodoa faida za mke mwema na hasara za mke mbaya

*        Kuntoa kile kinachotakikana kwa mke.                                        (2 x11/2  =  3)

 

(d)     *        Tarbia – mishororo minne

*        Mtiririko

*        Urari wa mishororo 16 kila mshororo                                                  (3 x 2 = 6)

 

  1. e) (i) Chachu – hasira / kitu kikali au kichungu

(ii)     Johari – kitu cha thamani / kizuri / uzuri wa mke

(iii)    Saburi – Subira / ungojevu / uvumilivu

(iv)    Mbishi – anayebisha

(v)     Pishi – kipimo cha vibaba vinne cha ratili/ upishi/ vitu / vyakula vilivyopikwa

( 5 x 1 = 5)

10.(a)          *       Ushujaa wa moyo

*        Bidii (2 x11/2  =  3)

(b)     *        Mtu asipokaza moyo wake, atapata kuwa vitu / mambo yote ni magumu

*        Mtu hataweza kupata mazuri / matamu maishani

*        Lakini mtu akijitahidi kwa kadri awezavyo, atapata kufaulu.            (Alama 4)

 

(c)     *        Mtu hataonja matamu / yaliyo mema hutapata

*        Ataishi na kuoza

*        Unalotaka halitawezekana

*        Uadui

*        Kila kitu kitakuwa kigumu                                                        (Hoja 3 x 1 =  3)

 

(d)     Vina – Ubeti wa tano vina vya mwisho ni ‘i’ lakini mshororo wa tatu ni ‘l’

Mizani – ni 8,  lakini katika baadhi ya beti ni 7, 8 au 8, 7                          (2 x  2  =  4)

 

(e)     *        Hakuamini ufanisi wake

*        Alikosa mtu mwingine wa kupigana naye                                  (11/2  x 2  =  3)

(f)      Akadiriki – akaamua / akaweza / akapata

Kushawishi – kumvuta mtu kwa maneno / pembeleza akubali

Kulidhibiti – tia mkononi / weza / linda au tunza.

 

KISWAHILI III

SEHEMU YA KWANZA

INSHA


Andika insha mbili zisizopungua maneno 350 – 400. Insha ya kwanza ni ya lazima.

 

  1. Umeteuliwa kuwa Mwanachama wa Kamati andalizi ya mkutano wa Harambee ya Kuwachangia vilema mkoani mwenu. Tayarisha ratiba itakayofuatwa katika mkutano huo.
  2. Bahati ni judi
  3. Nchi itaendelea ikiwa elimu itaimarishwa Jadili
  4. Ndoto ya ajabu

 

 

 

KISWAHILI

SEHEMU YA PILI

UFAHAMU, UFUPISHO, MATUMIZI YA LUGHA

 

Thamani ya shilingi ; tokea ibuniwe kama sarafu ya kuendesha biashara, inadunika kila kukicha. Tukirudisha nyuma gurudumu la wakati tutaweza kuchungulia na kujionea mengi ambayo yalikuwa yaweza kununuliwa kwa uwezo wa sarafu moja tu ya shilingi. Fungu la machungwa, au mkungu mzima wa ndizi au tita la kuni – haya yote yalikuwa yaweza kulipiwa shilingi tu kabla ya kumiliki kama mali yako. Kweli zama hizo, shilingi ingeweza kukushibisha na usilale na njaa.

Shilingi yenyewe ilikuwa na miujiza mingine. Thamani yake kwa miaka na miaka, ilikuwa ni ile ile na athara kama vile za kuanguka kwa thamani ya pesa ilikuwa ni jambo geni kabisa katika janibu hizi. Kwa wengi wa wakazi wa huku, athari hizo za kuanguka kwa thamani ya shilingi au Sarafu zozote zile za kilimwengu kama vile dola thabiti, yalikuwa ni matukio ambayo yalijulikana huku kama ndoto za vitabu vya historia tu. Ndoto hiyo leo ni ukweli mgumu usioaminika. Hali imewia kuwa ngumu zaidi na shilingi imekuwa chepechepe na ni shida kuitumainia kukunufaisha kwa chochote kile ila ukiwa na uraibu wa sigara moja mbili au ukiwa wataka kununua pipi tatu kwa kuondoshea ukakasi unaotokana na kuvuta sigara.

Shilingi ‘haingiari ikaua’ Enzi hizo zimepita na kamwe hazitarudi tena. Leo mifumo mbalimbali ya kiuchumi duniani imo katika gharika kweli kweli kwani adui ‘inflesheni’ amefaulu kuzizorotesha na kuziacha katika hali dhaifu viongozi mbali mbali kote duniani wakitawazwa, tamko lao la kwanza ni kupambana na adui huyu na kuingia  katika utawala wao na kujitolea kupambana naye adui huyo kama yumo katika vita vya kufa na kupona.

Uchumi mwingi umenyauka. Fikira na wataalamu wengi wenye kufahamu sayari ya uchumi wangali wamekaukiwa na mbinu za kumwagusha adui huyo ili maisha yarudie ile hali ambayo ilikuwa yadumu kila mahali ulimwenguni. Vitabu vya historia havisaidii kitu kwani fani yake adui huyu ilikuwa bado haija wakumba binadamu.

Usawazishaji wake ‘inflesheni’ wategemea mawimbi ya thamani za sarafu maalumu za kilimwengu. Wakati zinapokuwa makini na hazianguki kutokana na thamani zake, biashara na thamani ya shilingi zetu huwa pia shwari na zenye kurahisisha uendeshaji na upangaji wa biashara. Lakini mawimbi yake yakianza kugharikisha thamani za sarafu hizo, shilingi nayo huwa kama yalewalewa katika bahari ambayo haina upeo.

 

Maswali

  1. a) Toa tofauti mbili baina ya shilingi ya zamani na ya sasa ( alama 4 )
  2. b) Mwandishi wa taarifa hii alichochewa na nini hasa hadi akaandika ? ( alama 3 )
  3. c) Kuna ithibati gani kutoka taarifa kuonyesha kuwa kuanguka kwa thamani ya shilingi ni

tatizo     kubwa duniani ?                                                                            ( alama 4 )

  1. d) Mwandishi ametumia jazanda nyingi ili kusisitiza unyeti wa swala hili; kwa mfano …

tukirudisha nyuma gurudumu la wakati……… taja na uelezee jazanda nyingine

zozote mbili na uelezee maana ya kila moja                                              ( alama 4 )

  1. e) Kuna faida gani thamani ya sarafu maalumu ulimwenguni inapokuwa thabiti ? Toa

ithibati   zako kutoka taarifa                                                                        ( alama 2 )

  1. f) Eleza maana ya maneno haya kulingana na muktadha wa taarifa hii  ( alama 3 )
  2. i) Inflesheni
  3. ii) Janibu

iii) Mawimbi

 

MUHTASARI.

 

Katika kila kiwango, wanafunzi huonekana kama wana shida kubwa sana katika kuyachambua mashairi. Hali hii ni matokeo ya mambo mengi. Yaweza kuwa mashairi waliyokutana nayo mara ya kwanza yalikuwa magumu, au yalikuwa yamechanganya kiswahili sanifu na lahaja zingine ambazo wasomi hawangezielewa moja kwa moja.

Jambo hili huwakatisha wanagenzi tamaa hasa wanapokosa kulipata katika kamusi msamiati uliotumika. Wanapotamauku, wao huwa hawataki kujishughulisha na mashairi. Huu ndio mwanzo wa kuanguka kwao katika mitihani kwa vile wengi wao hulazimika kukutana na mashairi kwa mara ya kwanza katika chumba cha mtihani. Hiki ni kinyume cha jinsi mambo yanavyostahili kuwa. Ukweli ni kuwa mashairi yanastahili kuwaburudisha wasomi pindi wakutanapo nayo.

Madai kuwa mashairi ya kiswahili ni magumu kufahamika isipokuwa kwa watu maalum wenye vipawa maalum hayafai. Mwanafunzi ambaye anataka kufanya vizuri katika swali la mashairi ni lazima aanze kuyapenda mapema iwezekanavyo. Ni muhimu aazimie kuyapenda hasa ajuapo kuwa atatahiniwa katika sehemu hii. Kwa vile hana njia ya kuyaepuka, azingatie msemo wa wazungu usemao kuwa kama hupati upendacho, anza kupenda kile ukipatacho. Ili kuchochea upendo ndani yake, asijishughulishe na yale mashairi ambayo anayaona kama ni magumu. Ajaribu kuyaelewa yale ambayo anayaelewa na kuudondoa ule ujumbe ambao yameumbeba na vile vile ajaribu kuufurahia utamu wa maneno yaliyotumika. Atalipata hili kwa kuyasoma kwa sauti. Kila mara, akumbuke kwamba kadili atakavyokutana na mashairi mengi ndivyo atakavyofurahia na kuyaelewa.

Pili, akikutana na shairi, asishtushwe na msamiati au lahaja iliyotumika. Hata kama haelewi msamiati uliotumika, ajaribu kuelewa ujumbe uliomo katika shairi. Hata hivyo, lazima ajihami na msamiati mwingi iwezekanavyo. Isitoshe, ni muhimu katika mazoezi yake kujaribu kuandika mashairi yake mwenyewe ili aelewe ni kwa nini waandishi huyaandika mashairi jinsi wanavyoandika; Atagundua kwa nini waandishi huyarefusha, huyafupisha au huyabadilisha maana ya maneno mbali mbali.

 

Maswali.

  1. a) Ni mambo gani yanayochangia kuanguka kwa mwanafunzi katika swali la ushairi ?
                ( alama 7) ( maneno 40)

      Nakala Chafu.

      Nakala Safi.

 

  1. b) Mwandishi amependekeza hatua gani kuchukuliwa ili mwanafunzi afaulu katika

maswali ya mashairi ?                                                        ( alama 8 )  ( Maneno 50 )

     

      Nakala Chafu

      Nakala Safi

  1. c) Mwanafunzi ahitajika kufanya nini ili kuyapenda mashairi ( alama 5)

                                                                                                  ( maneno 20 )

      Nakala Chafu

      Nakala Safi

 

 

 

 

SEHEMU C: MATUMIZI YA LUGHA.

 

  1. a) Tumia kiulizi – pi katika kujaza sehemu zilizoachwa wazi. ( alama 4 )
  2. Ni tunda ____________ uliloleta ?
  3. Ni mayai ___________ yaliyovunjwa ?
  • Ni kiwete __________ aliyepata msaada ?
  1. Ni mitume __________ waliojilolea kufanya kazi ?

 

  1. b) Andika sentensi zifuatazo katika kauli ya kufanyisha / za ( alama 4 )
  2. Alikifanya kijiti kiingie ndani ya kufuli.
  3. ii) Mzazi alimfanya mwanawe alime siku nzima

 

  1. c) Tumia virejeleo vifavyo katika sentensi hizi.
  2. Mchezaji alipiga mpira kwa ustadi
  3. Simba alifukuza mtalii aliyetaka kupiga picha
  • Umeokota wapi ndizi hizi zote ?
  1. Andrea alipanga vizuri maua mezani

 

  1. d) Andika tena sentensi hizi ili zisiwe katika hali ya kukanusha ( alama 4 )
  2. Asiyekujua hakuthamini
  3. Asiyejua maana haambiwi maana
  • Fimbo ya mbali haiui nyoka
  1. Amani haiji ila kwa ncha ya upanga

 

  1. e) Ziandike sentensi hizi kwa kufuata maagizo
  2. Mlete mtu mwenye akili ( tumia ‘amba’ )
  3. Walifungana bao moja kwa moja katika mchezo ule ( tumia …… Sare )

 

  1. f) Unda majina kutoka vitenzi hivi ( alama 2 )
  2. i) Kulia _________________________ , Kudhani ______________________
  3. ii) Ni nini maana ya : Amepata ahueni                                              (alama 1 )

Amekuwa buge                                                                                   ( alama 1 )

 

  1. g) Andika sentensi ifuatayo katika udogo ( alama 2 )
  2. Alishikwa na jipu ambalo lilivimbisha dole lake la mguu mithili ya pesa
  3. ii) Akifisha sentensi hii: ( Alama 2 )

Ondiek aliita Maria Maria njoo hapa.

 

  1. h) Eleza matumizi ya ‘Ki’ katika sentensi hizi:
  2. Nitakapokuwa nikilala atakuwa akidurusu
  3. Kivulana hicho kinawafurahisha wenzake

 

  1. i) Andika maana mbili zinazojitokeza katika kila moja ya sentensi hizi
  2. Mwalimu alimsomea mwanafunzi
  3. ii) Alimlilia mwanawe
  4. j) Ikiwa Mtondo ni Jumamosi
    )   Juzi ni siku gani ______________________________                    (alama 1)
  5. ii) Leo ni siku gani ______________________________ (  alama 1)

 

 

iii)  Tunga sentensi mbili ukutumia tashbihi zinazotokana na maneno haya:

( baidika, mkizi)                                                                 ( alama10 )

 

SEHEMU YA TATU

USHAIRI.

 

  1. Mabadiliko lazima kwa watu ulimwenguni,

Nalo lilianza zama hakika si neno geni,

Ni tabia ya daima kipya kuwa cha zamani,

Kwa watu ulimwenguni mabadiliko lazima.

 

Kama hili halikuwa jipya lingekuja lini ?

Mfano wetu maua na majani mitini

Hili linapofumua, lile huanguka chini

Jipya lingekuja lini kama hili halikuwa

 

Kuwapo na kutowapo tumo mabadilikoni

Nakuapia kiapo kwamba hii ni kanuni

Nawe linganisha pepo kaskazi na kusini

Tumo mabadilikoni kuwapo na kutowapo

 

Tukitaka tusitake ni sheria tumo ndani

Waume na wanawake roho zote za manani

Kubadili mwendo wake dunia si yamkini

Ni sheria tumo ndani tukitaka tusitake

 

Mwendo wa dunia mbio haimo usingizini

Kwa aliye na kilio na aliye furahani

Mara huona machweo na mara jua kichwani

Haimo usingizini mwendo wa dunia mbio

 

Mbio maisha ya watu, mfululizo mbioni

Hali hii kila kitu, kilicho maumbileni

Mbio haingoji mtu – tuo haijulikani

Mfululizo mbioni, mbio maisha ya watu

 

Hutuchukua kwa zamu katika matumaini

Na mchungu na matamu hututokea njiani

Na mara hatufahamu lilikuwa jambo gani

Katika matumaini hutuchukua kwa zamu.

 

Maswali.

 

  1. a) Kuna mifano mingi ya kimaumbile iliyotolewa ili kudhihirisha dhana hii ya

mabadiliko. Itaje  mifano yoyote mitatu.                                                    ( alama 3 )

  1. b) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha nathari ( alama 4 )
  2. c) Kuna ithibati kuwa mabadiliko hayabagui ? ( alama 4)
  3. d) Nakili mishororo minne inayoeleza kuwa mabadiliko ni sharti maishani ( alama 4 )
  4. e) Katika shairi hili mwandishi ametaja maneno na vinyume vyao. Toa majozi manne ya

maneno  haya ( neno na kinyume chake )                                                   ( alama 2 )

  1. f) Eleza maana ya maneno yafuatayo:
  2. Linapofumua
  3. Kiapo
  • Tuo ( alama 3 )

 

  1. Nina machache muhimu, ambayo ni ya thamani,

Nataka kutakalamu, niyatoe hadharani,

Wayafahamu kaumu, marafiki ikhuwani,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Neno ‘UTU’ tufahamu, ni funzo kwetu soteni,

Nitawapa nidhamu, kwa mpango wa kanuni,

Na tena ni kwa nudhumu, kwa shauri kubaini,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Wema si mali ya mtu, hili tujue yakini,

Wala uzuri si kitu, wa umbo lako mwilini,

Kitu aula ni utu, kitu bora duniani,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Na kivazi na kitimo, kwa utu hakilingoni,

Nguo si kitu adhimu, na kiatu mguuni,

Kitu ni ubinadamu, kisokuwa na kifani,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Utu si kitu kujua, ujuzi wa akilini,

Ama alojaaliwa, kupata usultani,

Binadamu ni murua, ajuaye na hisani,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Utu ni adimu, kipawa chake manani,

Utu ni moyo rahimu, heshima yake insani,

Na tena ni ukarimu, na roho yenye imani,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Utu siyo ujabani, ushujaa wa vitani,

Mtu ni utu mzuri, wa tabia na makini,

Mwenye utu fahari, kwa wake na majirani,

Ewe kiumbe insani, kuwa mwenye utu.

 

Utu ni khulka njema, maumbile ya nyumbani,

Ni ubinadamu mwema, ni ya Mola yake shani,

Hima basi ndugu hima, utu ni wetu soteni,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Ya tisa ni kaditama, kalamu naweka chini,

Ikiwa niliyosema, nitakuwa makosani,

Tafadhali wa heshima, nawaomba samahani,

Ewe kiumbe insani, kuwa mja mwenye utu.

 

Maswali.

 

  1. a) Hili ni shairi aina gani ? ( alama 1 )
  2. b) Chambua shairi hili kwa kuzingatia:
  3. Mizani
  4. Vina ( alama 4 )
  5. c) Dondoa sifa halisi za utu kama zilivyotajwa katika shairi hili. ( alama 5 )
  6. d) Andika ubeti wa saba katika lugha ya nathari ( alama 4 )
  7. e) ‘…. Utu ni kitu adimu’ ………. Kifungu hiki kinamaanisha nini hasa ? ( alama 2 )

 

  1. f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika taarifa ( alama 4 )
  2. Kaumu
  3. Kubaini
  • Aula
  1. Soteni

 

KISWAHILI III

SEHEMU YA KWANZA

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA INSHA.

 

i.) MTINDO ( Kwa mfano swali la kwanza )

  • Mtahiniwa aweza kuandika ratiba kwa kufuata mtindo mwafaka. Ataja saa halafu kitendo kinacho fuata. Atumie lugha ya moja kwa moja isiyo na maelezo au fafamusi nyingi. Katika maswali mengi tumia mtindo wa kawaida
  • Sehemu zingine za usahihishaji yaani msamiati, maudhui, sarufi na hijai; tumia mtindo wa kawaida. Hapa chini ni mwongozo kama kielelezo tu. Tumia kielelezo hiki katika maswali yote.

 

  1. ii) Msamiati ( alama 5 )
  • Kadiria umbuji wake na kiwango cha lugha
  • Uafaka wa maneno ( sajili ) kulingana na muktadha
  • Kiwango cha kujitosheleza kimsamiati

 

iii) Maudhui                                                                                                    ( alama 5 )

  • Yaliyomo, yaani yale anayozungumzia katika insha yake yaweze kuoana na anwani.
  • Mawazo au hoja ambazo zimetajwa

 

  1. iv) Sarufi ( alama 6 )
  • Sehemu hii husahihishwa kwa kinyume na i.,ii na iii kwa sababu tunakosoa mwanafunzi na alama atakazopata zitategemea idadi ya makosa aliyofanya. Jumla ya makosa ya kuadhibiwa ni kumi na mbili ( 12 ), kila kosa likiwa na thamani ya nusu ( ½ ) alama.
  • Adhibu kila kosa la sarufi utakalopata kwa mara ya kwanza. Usirudie kuadhibu kosa lile lile mara mbili au zaidi ya moja.

 

  1. v) Hijai ( alama tatu za kuondolewa )

Kama ilivyo katika sarufi, sehemu hii hutegemea makosa yanayopatikana. Hukadiriwa kwa kutegemea idadi ya makosa sita ( 6 ) kila kosa likiwa na thamani ya nusu ( ½ ) alama.

KISWAHILI SEHEMU YA PILI

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

UFAHAMU.

 

  1. – Shilingi ya zamani ingeweza kununua vitu vingi ( ilikuwa na thamani ) lakini

shilingi ya  kisasa haiwezi  kunua vitu hivyo vyote.

–  Shilingi ya zamani thamani yake ilibaki hivyo hivyo lakini shilingi ya kisasa

inabadilika  kila wakati, inashuka ikipanda.                                                                             ( 2 x 2 = 4 )

 

  1. Amesumbuliwa na thamani ya shilingi inayoendelea kuzorota siku baada ya siku.

( alama 3 )

  1. – Uchumi mwingi kunyauka

– Mifumo mingi ya kiuchumi duniani imo katika gharika na imezoroteshwa na

inflesheni.                                                                                   ( 2 x 2 = 4 )

 

  1. – Uchumi umo katika gharika – uchumi umo katika janga / tatizo

– Uchumi umenyauka – uchumi umezorota

– Mbinu za kumwangusha adui – njia za kutatua tatizo fulani

– Mawimbi ya thamani – hali ya mambo kuhusu thamani ya sarafu

– Shilingi kulewalewa – kuanguka na kuongeza thamani – kutopata uthabiti.

( 2 x 2 = 4 )

  1. e) Biashara na thamani ya shilingi huwa shwari na hurahisisha uendeshaji biashara ( 2 )

 

  1. f) i.) Kuanguka kwa thamani ya shilingi
  2. ii) Eneo, mahali

iii) Mchafuko / kukosa ithabiti

 

 

MHUTASARI.

 

  1. – Shida ya kuchambua mashairi
  • Kuogopa mashairi baada ya kulikuta shairi gumu
  • Itikadi kuwa mashairi ni magumu
  • Kutofanya mazoezi na kukutana na mashairi kwa mara ya kwanza katika chumba cha mtihani
  • Kupata msamiati usiopatikana katika kamusi 5 x 1 = 5

 

  1. – Asivunjwe moyo anapokabiliana na mashairi magumu
  • Atupilie mbali dhana kuwa ushairi ni ngumu
  • Kuyapenda mapema na kufanya mazoezi
  • Ajaribu kutunga mashairi
  • Ajihami na msamiati              4 x 2 = 8
  1. – Akubali maana hana njia ya kuepuka
  • Ajaribu kufurahia utamu wa maneno
  • Asome kwa sauti
  • Apitie mashairi mengi              4 x 1 = 4

a + b + c  = 17             ( Utiririko = 3 )

 

 

SEHEMU C: MATUMIZI YA LUGHA.

 

  1. ) lipi
  2. ii) yapi
  • yupi
  1. wapi 4 x 1 = 4

 

  1. b) ) Alikiingiza kijiti ndani ya kufuli                                             ( 2 )
  2. ii) Mzazi alimlimisha mwanawe siku nzima                                 ( 2 )

 

  1. c) ) Aliupiga
  2. ii) alimfukuza

iii)  umeziokota

  1. aliyapanga

 

  1. d) ) Anayekujua anakuthamini                                                      ( 1 )
  2. ii) Anayejua maana huambiwa maana                                         ( 1 )

iii)  Fimbo ya mbali huua nyoka                                                    ( 1 )

  1. iv) Amani huja kwa ncha ya upanga                                            ( 1 )

 

  1. e) ) Mlete mtu ambaye ana akili                                                    ( 2 )
  2. ii) Walienda sare katika mchezo ule                                            ( 2 )

 

  1. f) ) Kilio / mlio , dhana                                                     ( 2 x 1 = 2 )
  2. ii) Amepata msaada / kupona kutoka ugonjwa                           ( 1)

Ameishiwa                                                                              ( 1 )

 

  1. g) ) Kilishikwa na kijipu ambacho kilivimbisha kidole chake cha kiguu cha pera( 2 )
  2. ii) Ondiek aliita “Maria! Maria! Njoo hapa”                               ( 2 )

 

  1. h) ) Hali ya kuendelea                                                                   ( 2 )
  2. ii) Udongo / kiambishi cha ngeli ya Ki – Vi                                ( 2 )

 

i.)   i.)   Mwalimu anasoma kwa niaba ya mwanafunzi

  • Mwalimu anasoma ili mwanafunzi asikie / aandike
  1. ii) Alilia kwa sababu ya mwanawe ( huenda kwa sababu mwana amepatwa na janga
  • Alimnyenyekea mwanawe ili ampe msaada

 

  1. j) ) Jumatatu                                                                      ( 1 )
  2. ii) Jumatano                                                                     ( 1 )

iii)  Kama ardhi na mbingu                                                ( 1 )

Mwenye hasira kama mkizi                                         ( 1 )

See also  Class 8 KCPE past papers, revision exams and made familiar handbooks free

 

 

 

 

 

 

SEHEMU YA TATU

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

USHAIRI.

 

  1. – Maana kufumua na kuanguka chini
  • Pepo kaskazi na wa kusi
  • Kilio na furaha
  • Machweo na macheo  ( 3 x 1 = 3 )

 

  1. – Maisha huenda yakibadilika, mara tunapatwa na machungu mara matamu, kila moja kwa wakati wake.                                                             ( 4 x 1 = 4 )

 

  1. – Watu ulimwenguni ( wote )

–   Waume kwa wanawake

  • Roho zote za manani
  • Aliye na kilio na aliye na furaha
  • Kila kitu kilicho maumbileni ( 4 x 1 = 4 )

 

  1. d) i.) Kwa watu ulimwenguni mabadiliko ni lazima
  2. ii) Ni sheria tumo ndani tukitaka tusitake

iii)    Tukitaka tusitake sheria tumo ndani

  1. iv) Nakuapia kiapo kuwa hii ni kanuni                             ( 4 x 1 = 4 )

 

  1. e) – Waume – Wanawake
  • Kaskazi – Kusini
  • Kilio –  furaha
  • Machungu –  Matamu                                                 ( 4 x 1 = 4 )

 

  1. f) – Linapofumua – linapotoa ua
  • Kiapo – kula yamini
  • Tuo –  kusita  ( sitama )                                              ( 3 x 1 = 3 )

 

 

KISWAHILI IV

SEHEMU YA KWANZA

INSHA

 

Andika Insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima. Insha ya pili chagua kutoka 2, 3, na 4. Insha zako zisipungue maneno 400.

Kila insha ina alama 20

 

  1. Toa maoni yako kuzishauri serikali za nchi za kiafrika jinsi ya kutumia vyema misaada wanayofadhiliwa na mataifa ya kigeni
  2. Mawasiliano yatakavyokuwa mwaka 2100
  3. Adui mpende
  4. Si lazima kusoma ili kufaulu maishani. Jadili

 

 

 

 

 

KISWAHILI SEHEMU YA PILI

UFAHAMU, MUHTASARI, MATUMIZI YA LUGHA

 

Yaonekana watu hawajali usanifu wa Kiswahili katika Afrika Mashariki kwa sababu hakuna chombo chenye uwezo wa kutoa uamuzi kuhusu istilahi na matumizi ya lugha. Katika Mashairi na tungo zingine umepenya katika riwaya na unazusha tisho kubwa kwa Kiswahili sanifu. Maneno Kama vile kua, tua, sikia na lia huandikwa na wengi kana ‘kuwa, tuwa, sikiya na liya.’

Matumizi ya lugha isiyo sanifu kama haya yaweza kuvumilika yakiwa katika lugha ya mazungumzo au ya mashairi. Maandishi sanifu na wastani yanatakikana kusisitizwa. Kukosa kutumia mtindo mmoja wa kuandika maneno ya Kiswahili kunazusha mawazo kwamba kila moja yuko huru kuandika kiswahili vile apendavyo. Ikiwa tunafanya bidii kuandika maneno ya kiingereza kama vile ‘saw’, ‘sew’, ‘sow’ na ‘soul’ kwa kutumia irabu inayotakikana ni kitu gani kinachotushawishi kuandika ‘sikiya’ badala ya ‘sikia’? Tunahitaji chombo chenye uwezo katika eneo zima la ulimwengu wa kiswahili ili kusuluhisha masuala kama haya.

Baadhi ya watu wanaweza kuwa na hofu kwamba kuanzishwa kwa Kamati au Baraza kama hilo kutaweza kuhatarisha hali ya kiingereza katika Afrika Mashariki, hasa katika Uganda na Kenya. Hofu kama hiyo haipaswi kuwepo kwa sababu kama nilivyoelezea, kusaidia matumizi ya kiswahili sanifu hakuizuii nchi kufuata sera ya lugha inayopendelea kiingereza vile vile ni wazi kwamba kiingereza si lugha ya Uganda, Kenya au Tanzania. Katika Afrika Mashariki kiingereza kitabaki kuwa lugha ya kigeni yenye umuhimu wa mawasiliano ya kimataifa na maandishi ya kitaaluma. Afrika Mashariki itaendelea kutumia kiingereza katika elimu ya juu na kuiwezesha kunufaika na maandishi ya kitaaluma na kiufundi.

 

MASWALI

  • Pendekeza anwani mwafaka kwa taarifa hii? (alama 2)
  • Kwa nini mwandishi anaona kuwa Kiswahili hakitiliwi maanani katika Afrika Mashariki? (alama 4)

(c)  Kinachohitajika ili kiswahili kiweze kuimarika ni nini?

  • Ni jambo gani hasa linalomshawishi mwandishi kuona kuwa Kiswahili sharti kiimarishwe?                                             (alama 3)

(e)  Unafikiri kilichochangia udunishaji huu wa kiswahili ni nini?                  (alama 4)

(f)    Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yaliyotumika katika taarifa     (alama 4)

  • Usanifu
  • Umepenya
  • Sera
  • Kielelezo

 

MUHTASARI

 

Babu na nyaya zetu waliweza kifundisha vijana mambo mengi na watu walikuwa wamenyooka sawasawa. Ilikuwa ni wajibu wa kila mzee kupitisha hekima yake kwa vijana kila mara kwa njia ya methali, vitendawili, shirikina na hadithi zenye mafundisho maalum. Mambo yote haya yaliwafanya vijana kuwaheshimu wakubwa kwa wadogo na watu wa marika yao. Watu walipokutana na wageni waliwaheshimu na waliheshimiwa. Ilieleweka kwamba neno ‘heshima’ lilikuwa la maana kwa kila binadamu na walijua kuwa heshima hainunuliki. Ilikuwa ni nadra sana kusikia zogo limetokea mahali popote.

Vijana wengi wa siku hizo walikuwa wakisifika kwa bidii, ushirikiano, uaminifu, utu, ukarimu, unyenyekevu, utiifu na upole. Wachache waliokosa sifa nyingi kati ya hizo walikosa wachumba. Hakuna aliyeweza kuficha tabia yake mbaya kwa muda mrefu kwa kuwa kila kijana pamoja na ndugu zake walifanya uchunguzi wa kutosha kabla ya kukubali posa. Upelelezi huu wa tabia ulianza tu mara mtu aliposema kuwa anataka jiko. Watu hawakujali ulemavu wa mtu na aghalabu waliokuwa na kasoro za kimwili waliweza kuoa ama kuolewa baada ya kuonekana kwamba wametimiza sifa nilizozitaja hapo awali.

Vijana walikubali kuelekezwa kutenda mambo mengi sana katika jamii bila ya maswali ama ubishi wowote. Hata walipoona mambo yamewawia magumu waliomba msaada kwa unyenyekevu mkubwa.

Hapo kale hapakuwa na mtindo wa vijana kupiga malapa mitaani. Waovu walikuwa wachache na waliweza kuadhibiwa na yeyote. Hakuna kijana aliyetoka kwao na kulala nje bila idhini ya wazazi wake na kama msichana angeweza kufanya hivyo, wazazi wangeweza kumlazimisha kurudi alipokuwa na arudi na huyo mtu aliyekuwa naye.

 

Maswali

  • Kulingana na taarifa hii, unafikiri ni mambo gani hasa yaliyochangia kuimarika kwa nidhamu kwa upande wa vijana? (Maneno 40) (alama 8)

      Nakala Chafu

      Nakala Safi

 

  • Eleza ujumbe unaojitokeza katika aya ya kwanza (maneno 40)                   (alama 6)

Nakala Chafu

      Nakala Safi

 

  • Fafanua aina za makosa na adhabu zilizotolewa hapo zamani kwa mujibu wa taarifa hii (maneno 30-35) (alama 6)

Nakala Chafu

      Nakala Safi

 

  1. MATUMIZI YA LUGHA.

 

  • Andika sentensi hizi kwa wingi (alama 4)

(i)  Buzi lililoibwa na jambazi lile limepatikana

(ii)  Mwenye kelele usidhani kapoa

 

  • Tunga sentensi ukitumia tashbihi zinazotokana na maneno yafuatayo
  • Gundi
  • Chiriku
  • Lumbwi
  • Wali wa daku

 

  • Kuna tofauti gani kati ya vyombo hivi
  • Dira / saa
  • Tofautisha maneno haya

(iii)       Sulubu / suluhu

 

 

 

  • Sahihisha sentensi hizi (alama 4)

(i)   Munyi alisanya vitabu yote siku ya Ijumaa

(ii)  Fupa huu ulivunjwa na mpwakoko hii

 

  • Andika sentensi ifuatayo bila kutumia neno ‘amba’

(i) Jembe ambalo lilinunuliwa jana limevunjika mpini                                    (alama 2)

  • Mwizi ambaye amekuwa akitusumbua ameshikwa

(alama 2)

  • Fuata maagizo uliyopewa katika kujibu yafuatayo

(i) Soma kwa bidii kijana. Utafaulu katika mitihani yako. (tumia …… nge)   (alama 2)

(ii) Kisu kinachonolewa ndicho kinachopata (geuza hadi hali ya mazoea) (alama 2)

 

  • Andika maneno mengine mawili yenye maana sawa na yafuatayo               (alama 4)

(i)         Daawa

(ii)        Bughudha

  • Abadani
  • Fitina

 

  • Kanusha sentensi hizi

(i)   Mwana yule alikuwa amekamilisha kuchimba mtaro alipojikata mguu

(ii)  King’ora kililia kioo kilipovunjwa

 

  • Weka viambisho vinavyofaa sentensi zifuatazo

(i)   Walimu ______ li ____ ona mtoto _______ dogo ________ kianguka matopeni.

  • Mwavuli huu __________ eusi __________ a mzungu ame _____________ nunua jana.

 

  • Andika sentensi ifuatayo katika kauli ya kufanyiza

(i) Mwalimu amefanya mwanafunzi wake ajue umuhimu wa bidii masomoni

(alama 2)

(ii) Paka ameyanywa maziwa (geuza hadi kauli ya kufanywa)                 (alama 2)

 

      SEHEMU TATU
      USHAIRI

 

  1. Tusitake kusimama, bila kwanza kutambaa,

Au dede kuwa hima, kabula hatuyakaa

Tutakapo kuchutama, kuinama kunafaa

Tujihimu kujinyima, makubwa kutoyauyaa

 

Tusitake kuenenda, guli lisipokomaa

Tujizonge na mikanda, inapochagiza njaa

Na mazuri tukipenda, ni lazima kuyaandaa

Tujiase kujipinda, kujepusha na balaa

Tusitake uvulana, au siga kuzagaa

Tushikaye nyonga sana, tunuiyapo kupaa

Kama uwezo hapana, tutoelee dagaa

Tujiase hicho kina, maji yajapokujaa

 

 

 

Tusitake vya wenzetu, walochuma kwa hadaa

Wanaofyatua vitu, na kisha vikasambaa

Uwezo hatuna katu, umaskini fazaa

Tujihimu kula vyetu, siendekeze tamaa

 

Mtaka kuiga watu, kufata kubwa rubaa

Vyao vijaile kwetu, vifaa vingi vifaa

Tunamezwa na machatu, tusibakishwe dhiraa

Tujihimu kilo chetu, hata kama twapagaa

 

Maswali

 

  • Lipe shairi hili anwani mwafaka (alama 2)
  • Chambua ubeti wa tatu na nne kwa upande wa vina na mizani (alama 4)
  • Thibitihsha jinsi kunga ya inkisari na mazida inayojitokeza katika shairi hili

(alama 3)

  • Mwandishi ana ujumbe gani katika shairi hili kwa wasomaji wake? (alama 2)
  • Andika ubeti wa kwanza kwa lugha ya nathari (alama 4)
  • Taja misamiati yoyote minne ya hatua ya maisha ya binadamu na ueleze yake.

(alama 4)

  1. Alikuwa mtu duni, alozongwa na shakawa

Hana alichoauni, wala alichoambuwa

Walikimwita mhuni, na thamani kumtewa

Utamwonea amani, jinsi ya alivyokuwa

Mwepesi wa kusahau

 

Alipita mtaani, kuomba kusaidiwa

Mtoto wa kimaskini, riziki haizumbuwa

Alizubaa njini, lake jua na mvuwa

Mwepesi wa kusahau

 

Ekosa kwenda chuoni, kwani alibaguliwa

Daima kawa mbooni, akitafuta afuwa

Chumia chungu mekoni, furaha kwake haiwa

Mwepesi wa kusahau

 

Wakati ukabaini, mjiuga akatambuwa

‘Katoka usingizini, napo kwenye kukawa

Watu wakamuamini, kuwa mtu wa mvuwa

Kumbe vile atahuni, na ujeuri kuingiwa

Mwepesi wa kusahau

 

Leo kawa Sultani, mwingine katu hajawa

Hatamani na haoni, nyuma aliyochukuwa

Anga kwake limeguni, gubi amegubiliwa

Mwanadamu maalum, hakika ukichinguwa

Mwepesi wa kusahau

 

 

Maswali

 

  • Eleza ujumbe unayojitokeza katika ubeti wa kwanza na wa pili (alama 4)
  • Fafanua maana ya kibwagizo katika shairi hili                  (alama 3)
  • Hili ni shairi la aina gani? Toa sababu (alama 2)
  • Je mwandishi amefaulu katika kuzingatia arudhi za utunzi? Fafanua (alama 6)
  • Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika taarifa (alama 5)
  • Alichoauni
  • Alizubaa
  • Ukabaini
  • Sultani
  • Maluum

 

KISWAHILI IV

SEHEMU YA KWANZA

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

INSHA.

 

Mtindo (alama 4)

  • Ni mpangilio wa insha kijumla: utangulizi, kiwiliwili na hitimisho
  • Ni mpangilio wa aya na sentensi katika kutenganisha hoja au mawazo mbalimbali
  • Ni unadhifu wa kazi

 

Msamiati (alama 5)

  • Ni umbaji na uandishi na usanii wa lugha
  • Matumizi ya msamiati kulingana na muktadha
  • Uzito wa lugha

 

Maudhui (alama 5)

  • Yaliyomo katika insha
  • Mawazo/hoja zinazoshihirisha ukweli wa anwani au zinazofafanua anwani hiyo

 

Sarufi (alama 6)

  • Usingatiaji wa kaida za lugha. Utumiaji wa lugha kitaalamu
  • Uakifishaji n.k
  • Kila unapopata kosa kwa mara ya kwanza liadhibu kwa kiondoa alama nusu (½) usiadhibu zaidi ya makosa kumi na mbili (12)

 

Hijai (alama 3 za kuondolewa)

  • Ni uendelezaji wa maneno
  • Kila kosa linapojitokeza kwa mara ya kwanza liadhibu kwa kuondoa alama nusu (½) usiadhibu zaidi ya makosa sita (6)

 

 

 

 

 

 

 

SEHEMU YA PILI

UFAHAMU, MUHTASARI, MATUMIZI YA LUGHA

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

 

UFAHAMU

  • Matumizi ya kiswahili
  • Uimarishaji wa lugha zetu
  • Utumiaji mbaya wa lugha ya kiswahili (alama 2)

 

  • Kinatumiwa kiholela bila uzingativu
  • Hakuna chombo chenye uwezo kutoa uamuzi juu ya matumizi ya lugha

(alama 3)

 

  • Kubuniwe chombo chenye uwezo wa kitoa uamuzi juu ya matumizi ya lugha hii
  • Kuanzishwa kwa kamati au baraza ya kiswahili (alama 3 X 1 = 3)

 

  • Kiingereza si lugha ya asili
  • Kiswahili ni lugha ya kiasili inayoendelea kutumika kote duniani (alama 3)

 

  • Imani kuwa kiswahili kinaweza kutumiwa kwa njia yoyote ile bila uzingativu
  • Sera ya lugha ya nchi nyingi zinapendelea kiingereza (alama 1½ X 2 = 3)

 

(f)  (i)   Usanifu – Usahihi, utumiaji lugha kwa njia sawa

(ii)  Umepenya – Umeingia/umesambaa

(iii) Sera – Mtindo wa kufuatwa

(iv) Kielelezo – Mfano                  (alama 4 X 1 = 4)

 

SEHEMU B: MUHTASARI

  • Babu na nyanya walifundisha vijana mambo mengi
  • Waliokosa kuwa na sifa nzuri walikosa wachumba
  • Uchunguzi wa kutosha ulifanywa dhihi ya tabia ya mtu
  • Vijana walikubali kuelekezwa
  • Adhabu ilitolewa kwa wale waliokosa

(alama 4 X 2 = 8)

 

  • Babu na nyanya kutunza vijana
  • Watu kuwa wamenyooka
  • Vijana waliwaheshimu wakubwa
  • Wageni waliheshimiwa
  • Ulikuwa nadra zogo kulokea

(alama 5 X 1 = 5)

 

  • Aliyekosa sifa nzuri alikosa mchumba
  • Kutoka kwao na kulala nje angerudishwa aende akalete huyo aliyekuwa naye (alama 2 X 2 = 4)

(a + b + c = 17, Utiririko = 3)

 

 

 

 

SEHEMU C: MATUMIZI YA LUGHA

 

(a)  (i)   Mabuzi yaliyoibwa na majambazi yale yamepatikana (alama 2)

(ii)  Wenye kelele msidhani kapoa (alama 2)

 

(b)  (i)   Hata kama fundi

(ii)  Kuwa na maneno mengi kama chiriku

(iii) Kuwa kigeugeu kama lumbwi

(iv) Kuadimika kama wali wa daku

 

(c)  (i)   Dira – huonyesha upande/hutumiwa na wasafiri kujulia wanakoelekea

Saa – chombo kinachoonyesha saa (alama 2 x 1 = 2)

 

(ii)  Sulubu – kazi ya kutumia nguvu/bidii/ushupavu

Suluhu – utatuzi, jibu (alama 2 x 1 = 2)

 

(d) (i)   Munyi alikusanya vitabu vyote siku ya Ijumaa (alama 2)

(ii)  Fupa hili lilivunjwa na mbwakoko huyu (alama 2)

 

(e)  (i)   Jembe lililonunuliwa jana limevinjika mpini (alama 2)

(ii)  Mwizi aliyekuwa akitusumbua ameshikwa (alama 2)

 

(f)  (i)   Ungesoma kwa bidii kijana ungefaulu katika mitihani yako (alama 2)

(ii)  Kisu kinolewacho ndicho hupata (alama 2)

 

(g)  (i)   Kesi/mashtaka

(ii)  Hasina/mori/ghadhabu

(iii) Katu/Kamwe

(iv) Porojo

 

(h)  (i)   Mwana yule hakuwa amekamilisha kuchimba mtaro alipojikata mguu (alama 2)

(ii)  Kingo’ra hakikulia kioo kilipovunjwa                                     (alama 2)

 

(i)   (i)   Walimu walimuona mtoto mdogo akianguka matopeni                     (alama 2)

(ii)  Mwavuli huu mweusi wa mzungu ameununua jana                           (alama 2)

(j)   (i)   Mwalimu amemjulisha mwanafunzi wake umuhimu wa bidii masomoni

(alama 2)

(ii)  Maziwa yamenywewa na paka                                                           (alama 2)

 

SEHEMU YA TATU

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

USHAIRI

 

(a)  Kujinyima

  • Kila jambo na wakati wake

(alama 1 x 2 = 2)

(b)  Vina: Ubeti watatu vina vya kati ni na, vina vya mwisho ni aa

Ubeti wa nne: vina vya kati ni tu na vya mwisho ni aa

Mizani: Kila mshororo ina mizani kumi na sita

Ukwapi mizani nane na utao mizani nane –8, -8,

(Vina hoja mbili 2 x 1 = 2)

(Mizani hoja mbili 2 x 1 = 2)

 

  • Inkisari – ufupishaji wa neno

Walochuma – waliochuma

Siendekeze – usiendekeze

Kilo – kilicho

            Mazida – urefushaji wa maneno

Kabula – kabla

(inkisari 2 x 1 = 2)

                        (Mazida 1 x 1 = 1 Jumla alama 3)

 

  • Tusijiinue/kujikaza kwa mambo ambayo hatujafikia

 

  • Tufuate mambo hatua kwa hatua kwa taratibu nzuri (alama 3 x 1 = 3)
  • Mtu asiwe na tamaa ya kusimama kabla hajatambaa au atake kusimama dede kabla hajaweza kukaa kitako. Ni heri kuanzia hatua za mwanzo halafu hatua zingine zifuate wala sio kinyume chake             (alama 4)

 

  • Kusimama – wima

Kutambaa – kutembea kwa magoti

Kusimama dede – kusimama bila kusaidiwa

Kukaa – kwa kitako

Kuchutama – chuchumaa, kaa kitako bila kugusa chini         (alama 4 x 1 = 4)

 

10.(a)   Mtu fulani hakuwa na sifa zozote nzuri mwenye shaka. Hana lolote

alichojupatia hata cha kupewa ikabidi kuona cha thamani kuwa duni. Afaa

kuonewa huruma kwa namna alivyokuwa                                          (alama 4)

 

      (b)  Mtu aweza kusahau yaliyofanyika kwa haraka                                  (alama 3)

 

(c)  Unne/tarbia – lina mishororo minne kila ubeti

Msuko –kibwagizo kimefupishwa                                          (alama 2 x 1 = 2)

 

(d) Ndio – idadi ya mishororo ni sawa kila ubeti (minne)

  • Mizani 16 kila mshororo isipokuwa katika kibwagizo ni nane
  • Vina vimetiririshwa (kuna urani) kina cha kati ni ‘ni’ cha mwisho ni ‘wa’ (alama 3 X 2 = 6)

 

(e) (i)         Alichosaidiwa

(ii)        Kutokuwa makini/bila tahadhari

  • Kuelewa
  • Kiongozi

(v)       Binadamu                                                        5×1=5

KISWAHILI V

SEHEMU YA KWANZA

INSHA

 

  1. Wewe ni katibu wa chama cha wakulima cha kiteka: Tayarisha kumbukumbu za

mkutano mliofanya hivi majuzi.

 

  1. Andika insha juu ya: Maisha yangu ifikapo mwaka wa 2020.

 

  1. Ndugu yako ameshtakiwa kwamba mnamo tarehe 12 Agosti mwaka jana, alipatikana

na hatia ya ulanguzi wa dawa za kulevya. Amekutaja kuwa ulikuwa na yeye wakati

huo nyumbani na umeitwa kutoa ushahidi juu ya:

alipokuwa wakati huo

Shughuli zake za kawaida

Historia yake

Maoni yako juu ya kesi hii.

Andika insha kuhusu vile utakavyomtetea mahakamani.

 

 

  1. Andika insha juu ya methali hii; Mtenda jambo asishe ni kama asiyetenda.

 

SEHEMU YA PILI

UFAHAMU, MUHTASARI, MATUMIZI YA LUGHA

 

SEHEMU A – UFAHAMU

 

  1. Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata:

Miaka michache iliyopita, kila aliyekuwa amesoma alikuwa na bahati ya kupata kazi katika ofisi za humu nchini. Wote waliofika darasa la saba au pengine kidato cha pili na zaidi wale waliofuzu mtihani wa kidato cha nne, walinyakuliwa juu kwa juu na wizara mbalimbali za serikali au pengine waliandikwa kazi na makampuni. Kwa vile kila moja wao alipata kazi ya kuajiriwa, hakuna aliyejishughulisha na kazi za mtu binafsi kama useremala, uashi, ukulima, uvuvi na kadhalika- kazi kama hizo ziliachiwa wale tu ambao hawakupata fursa ya kuenda shule.

Siku hizi mambo yamebadilika. Licha ya kuwa na elimu ya darasa la saba au kidato cha pili na pengine cha nne, hata wale wenye shahada za vyuo vikuu nao pia wamezifungia shahada hizo mashubakani zikiota ukungu huku wenyewe wakijipurukusha kulima au kufuga; na wale ambao bado hawajakata shauri kama hili, wako barabarani wakipiga lami.

Wakoloni walifanya kosa moja kubwa sana ambalo tumeligundua tu baada ya kunyakua uhuru wetu. Kosa lenyewe ni lile la kuwafanya wananchi waliopata elimu wasipende kushika kazi zinazochafua mikono.Walijua tu kwamba mashamba yao na hata mitambo yao ingalifilisiwa na ile ya waafrika; kwa hivyo ingaliwabidi hata wao waje wawatumikie wenyeji. Ndipo walipokata shauri kutowaamsha waliolala ili wasije wakalala wao.

Katika karne hii, wataalamu wameshawishika kuitumia elimu yao kufanya kazi za mashamba, ujenzi na ufundi wa mitambo. Ijapokuwa baada ya kazi kama hizo mikono huwa imejaa tope au masizi, pato lake ni kubwa ajabu. Jambo la kuvutia zaidi katika makazi kama haya ni kwamba mwananchi huwa ni ‘bwana’ mwenyewe, hujitegemea mwenyewe bila kochokocho.

Kila moja wetu yuaelewa kinaganaga kwamba kazi kama ya ukulima huleta donge kubwa zaidi ya kazi zote; kwani kila mfanyikazi humwelekea mkulima baada ya kumaliza kazi yake. Mkulima naye hutoa jasho jingi wakati wa kulima shamba. Baadaye atapekua magugu na visiki aviweke katika matita ili aviteketeze moto. Baada ya muda kidogo atapanda na angoje hadi mbengu zake ziaanze kuchipuza. Mara maua huchanua na mazao kujionyesha. Baada ya kuvuna, kazi yake kubwa huwa ni kuanika na kuanua nafaka zake. Wakati huo, mazao yake huwa yatanga, mara yuapanga mara yuapangua mipango juu ya uuzaji. Mazao yafikapo nyumbani, pengine mkulima huipamba nyumba yake na akawaita marafiki zake ili awakirimu kwa vyakula na vinywaji. Karamu ikiisha hana budi kupambua mapambo yote. Huyoo, aenda kuuza bidhaa zake; akirudi yuakaa raha mstarehe akila na kuburudika pamoja na familia yake. Je kuna kazi yenye raha zaidi ya ukulima?

Watu wengi hufikiria maana ya neno ‘kulima’ ni kushika jembe tu. Hiyo si kweli kwani kuna ukulima namna nyingi, kama vile ufugaji wa ng’ombe, mbuzi au kuku. Hata ufugaji wa samaki au utunzaji wa nyuki pia waweza kuitwa ukulima. Dhamira ya taifa letu changa ni kuwapatia mwangaza wananchi wake waliomo mashuleni, kwamba wangojewa kwa hamu wajiunge na wenzao katika kulijenga taifa lenye nguvu, ili katika kujisaidia wenyewe pia waongeze pishi katika kulipa taifa maongozi mema yasiyokinai kazi zilizokuwa zikiitwa ‘chafu’ lakini ambazo ndizo hasa kiini cha maendeleo na kujitegemea.

 

  1. a) Kulingana na habari uliyosoma, ni mambo gani hasa yaliyochangia kupuuzwa kwa

kazi za mtu binafsi?                                                                                 (alama 3)

  1. b) Wakoloni walikuwa na lengo gani kwa kufanya waafrika waliosoma kuchukia kazi za

mikono?                                                                                                   (alama 2)

  1. c) Unafikiri mwandishi wa taarifa hii alikuwa na dhamira gani kwa wasomaji wake?

(alama 2)

  1. d) ..‘Wamezifungia shahada hizo mashubakani zikiota ukungu huku wenyewe wakijipurukusha kulima au kufuga’ Mwandishi anamaanisha nini katika kauli hii?

(alama2)

  1. e) Kwa nini wasomaji wa kisasa wameanza kufanya kazi ya ukulima?        (alama 3)
  2. f) Eleza maana ya semi hizi kama zilivyotumiwa katika taarifa:                  (alama 4)
  3. i) Kata shauri
  4. ii) Kuwa bwana
  5. g) Mwandishi ametumia maneno yenye maana ya kinyume kwa mfano ‘panga na pangua’; yataje maneno mengine mawili yaliyotajwa na vinyume vyao huku ukieleza maana ya kila moja ya maneno hayo.                                             (alama 4)

 

  1. SEHEMU B MUHTASARI

Wataalamu wengi wamelieleza neno hili fasihi. Kwa hivyo fafanuzi na nadharia juu yake ni nyingi. Lakini hata hivyo, karibu wote wamehusika zaidi ama na fasihi maandishi.

Ukitazama fasihi kwa umbo lake la nje na umbo lake la ndani utaona kuwa ni taaluma inayojengwa na maneno, na maneno yenyewe hutumia fani maalumu za aina mbali mbali kutolea makusudi au maudhui ambayo humzingatia binadamu maishani… Japokuwa sanaa hii ya fasihi mara nyingine huzungumzia vitu, lakini hilo ni umbo lake la nje tu. Umbo lake la ndani hasa hujishughulisha na binadamu na ndiye kiini cha fasihi; ndiye shabaha yake.

Fasihi simulizi ni masimulizi tunayopokea mdomo kwa mdomo. Si masimulizi yaliyoandikwa tangu awali. Kwa ajili hii basi tutaona kuwa katika fasihi hii mna utumiaji wa ulumbi (ufundi wa kusema). Kwa vile chombo cha kutongolea fasihi simulizi ni mdomo, hapana budi kuwepo na mwenye huo mdomo, yaani msimulizi. Msimulizi huyo, anaposimulia anachosimulia, huwa na nafasi si ya kutumia mdomo wake tu kujieleza, bali hali, uso, mikono na mwili wake mzima. Nafasi hii mwandishi wa fasihi maadishi hanayo kwa sababu yeye, kinyume na msimulizi wa fasihi simulizi, huwa hanao mbele zake watu wa kumsikiliza au kumtazama. Badala yake yeye hupambana na msomaji.

Msimulizi katika fasihi simulizi ana nafasi ya kutazama kama amefaulu au la, yaani wasikilizaji wake wanamsikiliza au hawamsikilizi. Kama hawamsikilizi, basi huwa na nafasi ya kubadilisha mbinu wakati huo huo asimuliapo ili wamsikilize. Na hapo ndipo aonyeshapo ufundi wake katika sanaa ya usimuliaji. Lakini nafasi hiyo mwandishi hanayo anapoandika.

Tena msimulizi ana nafasi ya kuwatumia wasikilizaji wake kama wahusika asimuliapo ayasimuayo. Hii ndiyo sababu msimulizi aweza kumfinya mtu, kuigiza jambo, au kuwafanya watu waimbe, au kufanya matendo mbalimbali mengine. Ufundi na nafasi hiyo ni waandishi wachache wanaoimudu na kuitumia maana huhitaji umahiri wa hali ya juu. Kwa njia hii msimulizi kwa upande mmoja huwa na wahakiki palepale, hali mwandishi ni mpaka andiko lisomwapo ndipo anapoweza kuwapata.

Kwa upande mwingine, fasihi simulizi ina wasikilizaji zaidi kuliko wasomaji; wasikilizaji ambao mara nyingi waweza kuwa wahusika wa jambo linalosimuliwa. Wao wana nafasi ya kuuliza maswali, kuonyesha hisi zao, kuhimiza, kukumbusha, na hata kujibizana na msimulizi. Msomaji hana nafasi ya aina hiyo asomapo andiko.

 

  1. a) Pendekeza anwani mwafaka wa taarifa hii. (alama 2)
  2. Kwa kutumia maneno yasiyopungua kumi(10) wala kuzidi ishirini(20), eleza maana na lengo la fasihi kama ilivyotolewa katika taarifa.                                (alama 4)

Nakala chafu

Nakala safi

 

c)Mpokezaji wa fasihi andishi ana vikwazo gani akilinganishwa na yule wa fasihi simulizi?     (maneno 70-80) (alama10)

Nakala chafu

      Nakala safi

 

  1. d) Wapokeaji wa fasihi simulizi wanawezaje kuathiri uwasilishaji wa fasihi?

(maneno 20)   (alama 4)

Nakala chafu

Nakala safi.

 

  1. 3. SEHEMU C: Matumizi ya lugha:

 

  1. a) Andika sentensi zifuatazo katika hali ya umoja.
  2.   i) Mkitusaidia, nasi tutawanunulia zawadi nzuri.                                      (alama 2)
  3. ii) Waliposikia sauti hizo, waliwarushia mawe hadi wakafa.                    (alama 2)
  4. b) Eleza maana mbili zinazojitokeza katika sentensi hii.
  5. i) Alifuatwa hadi akashikwa na mmeo dukani.                                       (alama 2)
  6. ii) Kuna tofauti gani kati ya sentensi hizi?

Ukirudi tena, nitakuadhibu vilivyo.

Ukirudi, tena nitakuadhibu vilivyo.                                                     (alama 2)

 

  1. c) Sahihisha sentensi hii bila kubadilisha maana.
  2. i) Mkutano ulihairishwa hati ijumaa. (alama 1)
  3. ii) Fuata maagizo uliopewa katika kujibu swali hili.

Wananchi walimpokea mjumbe kwa shangwe na vigelegele. (Tumia.. pokelewa).

(alama 2)

  1. d) Igawe fungutenzi ifuatayo kwa kubainisha kila sehemu huku ukionyesha na kufafanua maana ya visehemu hivyo vinavyounganishwa ili vifanye sentensi kamili.                   (alama 6)

         Alikiangusha

  1. e) Tunga sentesi ukitumia maneno yafuatayo ili kudhirisha tofauti ya maana kati yao.
  • (alama 3)

(i)  bovu                         (iii) bofu

(ii) pofu

 

  1. f) Chagua neno ambalo haliambatani na mengine.
  2. i) nyerere, ushanga, bangili, shimere.                                                        (alama 1)
  3. ii) bunga, punguani, mkatili, baradhuli.                                                    (alama 1)

iii) Unganisha sentensi hizi ili ziweze kuwa sentensi moja.

  1. Kelvin ni mwadilifu
  2. Kelvin aliteuliwa kuwa kiongozi.                                             (alama 2)

 

  1. g) Eleza maana ya misemo hii
  2. i) Shika sikio.                                                                                            (alama 2)
  3. ii) enga enga mtoto.                                                                                  (alama 2)

 

  1. h) Andika upya sentensi hii kwa kuandika neno lenye maana sawa na lile lililopigwa mstari.
  2. i) Mfalme yule alighadhabika alipofedheheshwa na watumishi wake katika karamu

ile.                                                                                                                    (alama 1)

  1. ii) Andika upya sentensi hii kwa kuandika kinyume cha kila neno lililopigwa mstari

Wifi alipovaa nguo na kusimama, ajuza yule alikaa.                      (alama 2)

 

  1. i) Andika sentensi hii katika hali ya udogo .
  2. i) Mtoto mdogo alipatikana ndani ya nyumba ile.                                    (alama 2)
  3. ii) Eleza maana ya PO kama ilivyotumiwa katika sentensi hizi. (alama 2)

Wanafunzi wachelewapo, huchapwa viboko vinne.

Wanafunzi wanapochelewa, huchapwa viboko vinne.

 

  1. j) Andika sentensi ifuatayo kwa wakati uliopo.
  2. i) Yusuf hakulima shamba lake. (alama 1)
  3. ii) Andika sentensi hii katika msemo halisi.

Mariam alimshukuru Edith na kutaka kujua wakati aliporudi kutoka nyumbani.

(alama2)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

  1. SEHEMU TATU

      USHAIRI

 

  1. Siku moja itafika, nijifungie safari;

Safari ndefu hakika, isiyotaka magari;

Magari hayatafika, wala meli za fahari;

Siku yangu!

 

  1. Siyo nadhiri naweka, katu siyo ubashiri;

Ni mwendo uliopangika, ni muhali kughairi;

Kwenda nawajibika, kubeta sina hiari;

Siku yangu!

 

  1. Roho inanitutika, kila nikitafakari;

Ziara is’o shirika, hata akhi hujibari;

Wanabaki kuteseka, na kunipami kwaheri;

Siku yangu!

 

  1. Siku itakapofika, zamani za kuabiri;

Kutazuka hekaheka, kibuhuti cha Suduri;

Na mwingi mno wahaka, kwa wendani na wambari;

Siku yangu!

 

  1. Ziara itafanyika, na mola ndiye Sayari;

Ngia itanimulika, nifike pasi usiri;

Niwache mkitamka, mabayangu na mazuri;

Siku yangu!

 

  1. Binadamu hutoweka, siku yake ikijiri;

Ugeni una mipaka, nami leo nahajiri;

Mipaka yangu yafika, mungu amenihitaji;

Siku yangu!

 

  1. Sina budi kuitika, wito huu wa kahari;

Ziara kukamilika, moyoni sifanyi ari;

Nenda zangu haraka, moyoni sifanyi ari;

Siku yangu!

 

  1. Haki sasa naondoka, ni mja sina hiari;

Huko nitasetirika, dahari hata dahari;

Buriani wahibaki, na maswahaba kwaheri;

Siku yangu!

 

Maswali:

  1. a) Mtunzi wa shairi alikuwa na dhamira gani katika kutunga shairi hili?     (alama 3)
  2. b) Idhini ya ushairi/ mtunzi inajitokezaje katika shairi hili?                          (alama 4)
  3. c) Kwa kutumia ithibati kemkem (kutoka katika shairi hili), eleza kwa undani muundo

wa shairi  hili.                                                                                            (alama 4)

  1. d) Eleza ujumbe unaotolewa na mwandishi katika ubeti wa saba na nane. (alama 4)
  2. e) Mafungu yafuatayo yametumiwa kumaanisha nini?
  3. i) ni muhali kughairi.                                                                               (alama 1)
  4.   ii)  ziara is’o shirika.                                                                                (alama 1)
  5. f) Toa mifano miwili ya jazanda katika utunzi huu. (alama 3)

 

  1. Mtu na awe na macho, kamili yote mawili,

Na kila kitu ambacho, alikiumba Jalali,

Kama hana kichwa kwacho, si mtu bali tumbili,

Kichwa ni yeye wakili, wa kila kitu mwilini.

 

Wa kila kitu mwilini, ni yeye huwa wakili,

Na yeye ndiye mashini, ya kuendesha kauli’

Kito cha matumaini, usukani wa akili,

Kichwa ni yeye wakili, wa kila kitu mwilini.

 

Wakili wa kila kitu, viungo vyote vya mwili,

Kichwa kinaleta utu, kwa sifa ya taamuli,

Ama ufanywe utu, kwa sifa ya taamuli,

Kichwa ni yeye wakili, wa kila kitu mwilini.

 

Mtu huwa ni sanamu, hajaumbika kamili,

Kama hanayo fahamu, fahamu yake thakili,

Si kichwa cha binadamu, binadamu wa asili,

Kichwa ni yeye wakili, wa kila kitu mwilini.

 

Tazama mwendawazimu, kichwa kilotanakali,

Huingiwa na zahamu, kukiuka ya awali,

Mfano wa marehemu, kila kiungo hajali,

Kichwa ni yeye wakili, wa kila kitu mwilini.

 

Kichwa chenyewe si hoja, hoja ubongo mkali,

Kiwe kijua vioja, kwa kamili atikali,

Si kichwa chenye kuvuja, si kichwa chenye manzili,

Kichwa ni yeye wakali, wa kila kitu mwilini.

 

Kichwa kiwe peke, juu ya kiwiliwili,

Shingoni ukitungike, na nywele kama ulimi,

Moyo visiunganike, kichwa hakitahimili,

Kichwa ni yeye wakili, wa kila kitu mwilini.

 

Maswali:

  1. a) Fafanua ujumbe unaobebwa na kiitikio cha utungo huu.                        (alama 3)
  2. b) Andika ubeti wa sita katika lugha nathari. (alama 4)
  3. c) Mja asiye na ‘kichwa’ amefananishwa na nini? Toa mifano miwili.        (alama 2)
  4. d) Ingawa kichwa ni muhimu, ni sharti kishirikishwe na viungo vipi ili kipate ukamilifu

wake?                                                                                                        (alama 3)

  1. e) Shairi hili ni la bahari gani? Toa sababu. (alama 2)
  2. f) Eleza mpangilio wa vina katika ubeti wa pili. (alama 2)
  3. g) Taja na ueleze maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi.
  4. i) Neno la mwisho katika utao wa mleo ubeti wa kwanza. (alama 2)
  5. ii) Neno la mwisho katika ukwapi wa mwanzo ubeti wa tano.                (alama 2)
See also  Geography Notes Form 1-4 Latest

 

SEHEMU YA KWANZA

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

INSHA.

 

  1. Kila insha ina alama 20-jumla-40
  2. Tumia mtindo huu kukadiria alama
  3. a) Maudhui -5
  4. b) Mtindo -4
  5. c) Sarufi -6
  6. d) Msamiati – 5     

20

Tajilia  -3

 

  1. MAELEZO
  2. a) Maudhui

 – Ni mada au maelezo au vipengele ambavyo mtahiniwa anahitajiwa kutaja katika insha

yake

– Mwanafunzi ataje mawazo au hoja zinazooana na anwani ya insha yake. Namna ya

kutunza:-

Ikiwa ametaja hoja zote –5

Ametaja zaidi ya nusu    -3½

Ametaja chini ya nusu    -2

Hakutaja chochote          -0

 

  1. b) Mtindo

Ni mpangilio wa insha –Utangulizi, maelezo ya mwisho / hitimisho.

Namna anavyotoa mawazo yake na jinsi anavyotiririsha.

Namna anavyojenga insha yake na umbo lake kijmla

Tuzo:    Hutegemea mambo yaliyotajwa hapo juu

                  Mtahiniwa hapewi 0

 

  1. c) Sarufi

Ni matumizi ya lugha kulingana na kaida za kisanifu.

Namna inavyotoa mawazo yake na jinsi anavyotayarisha

Matumizi ya nyakati, minyambuliko, herufi kubwa na ndogo / nakifishaji, kutenganisha, au kukutanisha maneno, n.k.

Namna ya kutunza:

Kwa kila kosa la sarufi, ondoa alama ½, Usiondoe zaidi ya nusu  12 kwani insha moja yaani.               (alama 6)

Kosa moja likitokea, liadhibiwe au kutolewa alama ½  lakini kosa hilo likirudiwa, linakosolewa  tu bali alama ½ haiondolewi.

Jumla ya alama za kisarufi zilizopatikana huhesabiwa na kuondolewa kutoka 6.

Mfano:- yaani ikiwa umepata makosa manne itakuwa ½  x 4 = 2

Tuzo itakuwa 6 – 2 = 4

 

 

 

 

 

  1. d) Msamiati:

Ni utumiaji wa msamiati wa lugha ya kiswahili ipasavyo. Ni uzito wa lugha ya mwanafunzi

Tuzo: Huweza kukadiliwa kwa daraja tatu:-

Juu ya wastani.

Wastani.

Chini ya wastani.

Mtahiniwa hapewi 0

 

  1. e) Tahajia au hijai

Makosa ya tahajia ni maendelezo mabaya ya maneno.

Tuzo:- Ondoa alama ½ kila unapopata kosa la tahajia. Kosa linaporudiwa, usiondoe alama kwa mara ya pili, kijumla usiondoe zaidi ya alama ½ (6) yaani alama 3 katika insha moja.

Mfano wa namna ya kutuza kijumla

Maudhui        – Ametaja zaidi ya nusu     -4

Mtindo          – Juu ya wastani                 -3

Sarufi            – Makosa 9 x ½  = 4 ½       – 6 – 4 ½  = 1 ½

Msamiati       –  Juu ya wastani                -3

Tahajia          – Makosa 3 = 3 x ½ = 1 ½

 

 

= Maudhui    -4

Mtindo       -3

Sanifu       -1 ½

Msamiati   -3

Jumla = 11 ½ – 1 ½  (Tahajia) = 10

Alama 10/20

Baada ya kujumlisha na kuondoa alama za tahajia, Iwapo kuna nusu yake, hujazwa

kuwa alama  kamili.

K.m.  10 ½ / 20  = 11/20

 

 

SEHEMU YA PILI

MATUMIZI YA LUGHA, UFAHAMU, MUHTASARI

MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

 

UFAHAMU.

 

1.(a) Kuajiriwa na wizara mbalimbali za serikali kwa urahisi (kwa wale waliopata elimu):

Kuandikwa kazi na makampuni

Wakoloni walifanya kosa la kufanya waliosoma kuchukia kazi za mikono.

Hoja zote tatu 3 x 1 = 3

 

(b)  Walijua kwamba kama waafrika wangefanya kazi za binafsi / mikono, ingefilisha mashamba yao (ya wakoloni) kwani waafrika hao wenye elimu wangetumikia wenyeji.           1 x 2 = 2

 

 

 

(c)  Anawatahadharisha wasomi dhidi ya kuchukia kazi za binafsi na kutarajia kuajiriwa. Anawataka wawe tayari kujitegemea baada ya kupata elimu.                     (alama 2)

 

(d) Anamaanisha kwamba watu waliopata shahada hawapati kazi za ofisi na hivyo huwajibika kufungia shahada hizo zao masandukuni na kuanza kufanya kazi za kibinafsi kama kulima, useremala n.k.

Shahada hizo haziwafaidi kwa vyovyote maana haziwasaidii kujipatia riziki.

Hoja moja  1 x 2 = 2

 

(e)  Kazi ya ukulima ina pato kubwa – donge kubwa zaidi ya kazi zote.

Kazi za kuajiriwa zimekuwa nadra kupatikana.

(Hoja zote mbili alama 3)

 

(f)  i.) Kata shauri – amua

  1. ii) kuwa bwana – kuwa wa kuheshimiwa, wa kutegemewa na mwenye hadhi.

(2 x 2 = 4).

(g)  –   Kuanika na kuanua.

–    Pamba na pambua.

–     Kuanika – weka juani ili (nafaka) ikauke.

–     Kuanua – kusanya (nafaka) ili ipelekwe ndani baada ya kukauka.

–     Pamba – kuweka nyumba kuwa katika hali nzuri (kwa mapambo).

–     Pambua – kuondoa mapambo yaliyokuwa yamewekwa nyumbani baada ya

karamu.                      1 x 4 = 4.

+ 4 + 4 = 20.

 

MUHTASARI.

 

  1. a) Fasihi simulizi – au anwani yoyote mwafaka (alama 2)
  2. b) Fasihi ni taaluma inayojengwa na maneno ambayo hutumia fani mbalimbali.

Hushughulikia binadamu na ubinadamu wake maishani

Hoja mbili = 2 x 2 = 4

Ondoa alama moja (1) anapozidisha maneno matano juu ya ishirini.

 

  1. c) – Hana nafasi ya kutumia viungo vingine vya mwili au ishara kufaulisha mawasiliano

–     Hana nafasi ya moja kwa moja ya kujifathrini kama amefaulu au la

–     Hana nafasi ya kuwatumia wapokeaji wa kazi yake

–     Hadhira au wapokeaji wa kazi yake ni ndogo.

Hoja zote nne = 2 x 4 = 8 ;  Utiririko = 2  ;  Jumla = 2 + 8 = 10

Ondoa alama moja (1) kwa maneno kumi yanayozidishwa usiondoe zaidi ya

 alama 3.

 

  1. d) – waweza kuwa wahusika.

–     wana nafasi ya kuuliza maswali.

–     waweza kuonyesha hisia zao.

Hoja tatu – 1 x 3 = 3  ;  Utiririko – alama 1   ;   Jumla = 1 + 3 = 4

Ondoa alama 1 idadi ya maneno inapozidishwa kwa maneno tano juu ya ishirini.

Usiondoe zaidi ya alama mbili.

            Jumla  2 + 4 + 10 + 4 = 20.

 

 

 

MATUMIZI YA LUGHA.

 

  1. a) Ukinisaidia, nami nitakununulia / nitamnunulia zawadi nzuri. (alama 2)
  2. b) Aliposikia sauti hiyo, alimrushia jiwe hadi akafa. (alama 2)
  3. c) i) Mume wake ndiye aliyemshika huyo (bibi) dukani.

Aliyekuwa akifuatwa (bibi) alishikwa pamoja na mmewe dukani.      (1 x 2 = 2)

  1. ii) – Mtu anaonywa asirudi, maana akifanya hivyo (kurudi) ataadhibiwa.

Ya pili – Mtu anaonywa kuwa akirudi, ataadhibiwa mara nyingine (kama alivyoadhibiwa awali) – Tayari ameadhibiwa. (1 x 2 = 2).

 

  1. d) i) Mkutano uliahirishwa hadi i (alama 1)
  2. ii) Mjumbe alipokelewa na wananchi kwa shangwe na vigelegele. 1 x 2 = 2

 

  1. e) ) A/li/ki / angu/sha

A- kiwakilishi cha nafsi (ya tatu) – yeye.

Li –kiwakilishi cha wakati (uliopita)

Ki – kirejeleo cha ngeli ya KI – Vi (umoja) inarejelea

Kitu – kitendwa.

Angu – shina la kitenzi.

Sha – Hali ya kutendesha.

Kugawa vizuri sehemu zote – alama 1

Kueleza / kubainisha visehemu 1 x 5 = 5

Jumla 1 + 5 = 6.

 

  1. e) (i) bovu – kilichooza, kisicho na thamani

(ii) bofu – mfuko wa mkojo tumboni

(iii) pofu – asiyeona.

*sentensi yoyote sahihi maadam maana zilizotajwa hapo juu zijitokeze waziwazi.

            1 x 3 = 3

  1. f) i) Shimere ii) mkatili
  2. g) i) kukataza mtu jambo fulani – kama daktari anavyowakataza watu vyakula fulani

kutengemea ugonjwa.

  1. ii) enga enga mtoto – kumdekeza mtoto.

kutomuadhibu hata anapostahili kuadhibiwa.

Kumpatia vyovyote atakavyo.                           2 x 2 = 4.

 

  1. h) Mfalme yule alikasirika alipoaibishwa na watumishi wake katika karamu ile.

* Neno lingine lenye maana sawa (visawe) na lile lililotajwa likubaliwe.

Sahihisha ukamilifu wa sentensi – hakuna kupata nusu – (alama 1)

  1. ii) Shemeji alipovua nguo na kukaa, buda yule alisimama (kama hapo (i.) alama

 

2.i) Kijitoto / kitoto kidogo kilipatikana ndani ya kijumba kile.  (Alama 2)

Po – katika sentensi ya kwanza inaonyesha mazoea yaani kila wakati akifanya

hivyo   (kuchelewa).

Po – katika sentensi ya pili inaonyesha wakati maalum – pindi tendo hilo

(kuchelewa)  linapotokea.            1 x 1 = 2

  1. ii) Yusuf halimi shamba lake. 1 x 1 = 1

iii) “Asante Edith” Miriam alimshukuru. “Na ulirudi lini kutoka nyumbani?”

Miriam alimwuliza (Edith)

“Asante” Miriam alimshukuru Edith; Ulirudi lini kutoka nyumbani? Miriam

alimwuliza Edith.

“Asante sana Edith; ulirudi lini kutoka nyumbani?” Miriam alimwuliza.

* Tazama jibu hili na upime kama itakubalika vilevile.                       2 x 1 = 2

Jumla 40

 

SEHEMU YA TATU

USHAIRI.

 

  1. a) Mtunzi aeleza kuhusu siku yake ya kuondoka ulimwenguni siku ya kufa kwake. Kwamba siku hii ni sharti ije haiwezekani kuepukwa.                        (alama 3)

 

b    Mtunzi anakutanisha maneno mawili.

Mabayangu – badala ya – Mabaya yangu.

Is’o amefupisha badala ya Isiyo.                                                  (2 x 2 = 4)

 

  1. c) – Ni tarbia – Mishororo minne kila ubeti

umeumbwa kufuata mtindo wa msuko – mshororo wa mwisho umefupishwa.

Aina ya mtiririko, vina vya mwisho ni sawa toka mwanzo hadi mwisho ‘ri’, kina cha kati vile vile kimetiririshwa ‘ka’ isipokuwa katika ubeti wa nane / mwisho.

Hoja zozote mbili – 2 x 2 = 4.

 

  1. d) Katika ubeti wa saba, mwandishi akiri kwamba anaungama na kukubali kuitwa na mungu maana maisha yake yamefikia mwisho hawezi kughairi. Ana enda zake yaani mapumzikoni ya milele.

Katika ubeti wa nane yeye asema kuwa kwa vile yeye ni binadamu, hana la kuchagua, kwa kufanya hivyo, huko aendako atahifadhiwa na kulindwa milele. Anahitimisha kwa kuwaaga wanaobaki.

 

  1. e) i) Ni muhali kughairi – Haiwezekani kwenda kinyume au kupindua.
  2. ii) Ziara is’o shirika – ni safari au mwendo ambao hakuna wa kukusindikiza au kuandama nawe. Ni safari ya mtu binafsi – pekee.

 

  1. Siku ya kufunga safari ndefu – siku ya kuacha dunia.

Ziara is’o shirika – siku ya mauti hujia mtu pekee kila moja na wakati wake.

1 ½  x 2 = 3                 Jumla 3 + 4 + 4 +4 + 1 + 1 + 3 = 20

10.a) Kichwa au hasa ubongo ndio unaoamua na kupanga kila kitu mwilini. Ubongo ndio unaoweka mizani na kutolea amri sehemu zingine za mwili.                 (alama 3)

 

  1. b) Kilicho muhimu ni ubongo wala sio kichwa hasa. Sababu ni kwamba ubongo ndio ulio na uwezo wa kujua mambo mengi yaliyokamilika sio kiungo kichwa. Inatakikana kile ambacho hakivuji mambo.              (Alama 4)

 

  1. c) Amefananishwa na: 1) Sanamu            2) tumbili                                                                      (alama 2  1 x 2 = 2)

 

  1. d) Kishirikisho na: – shingo.

nywele

moyo                     1 x 3 = 3

 

  1. e) Tarbia / unne – Mishororo minne kila ubeti.                                             (alama 2)
  2. f) – Vina vya kati (ukwapi) katika mishororo mitatu ya mwanzo (mwanzo, mtoto, mleo) kina ni ‘ni’ katika kibwagizo kina ni

kina cha mwisho (utao) katika mishororo mitatu ya mwanzo (mwanzo, mtoto na mleo) ni ‘li’ isipokuwa katika kibwagizo kina ni ‘ni’

Hivyo shairi katika ubeti huu unafuata mtindo wa ukara

Kielezo __ni,  ___li.

___ni, ____li.

___ni, ____li.

___ni, ____li.

Maelezo ya kina cha ukwapi – alama 1 ;  Utao – alama 1

 

  1. g) i) Jalali – jina la Maulana, mwenyezi mungu.
  2. ii) Mwendawazimu – Mtu aliye na matatizo ya akili asiye na akili timamu, anayeweza

kuleta madhara.            (1 x 2 = 2)

Kutaja maneno haya mawili kisahihi ni alama moja kila moja.

Maelezo sahahi ya maneno haya ni alama moja kila moja.

Jumla 1 + 1 + 1 + 1 = 4.

      Jumla swali zima 3 + 4 + 2 + 3 + 2 + 2 + 4 =20

 

KISWAHILI VI

SEHEMU YA YA KWANZA

INSHA.

 

  1. “Hamjambo wanafunzi . Ninamshukuru mwalimu mkuu kunialika kuja ili niwafahamishe kuhusu ukimwi …….” Endeleza hotuba hii mpaka mwisho .
  2. Mti ukifa shinale na tanzuze hukauka .

Toa hoja zitakazounga mkono usemi , ‘Katika jamii za kiafrika mwanamke angali anadunishwa’

  1. Eleza shida zinazoikumba nchi hii na upendekeze suluhisho zinazoweza kutolewa.

 

SEHEMU YA KWANZA

MWONGOZO  WA KUSAHIHISHA,

INSHA.

 

Maudhui

Chanzo

 (i) Kufanya   mapenzi na  mtu aliye na  virusi vya   H.I.V

(ii) Kwa  kutumia  vifaa  kama  sindano ,  wembe  .

(iii) Kuongezwa  damu  iliyo na   virusi  vya   H.I.V

(iv) Kubusiana .

 

Kinga 

(i)  Kuwa  na  mpenzi  mmoja  ( asiye na  virusi  vya  H.I.V)  aliye   mwaminifu  kwako.

(ii) Kutumia mipira  ikiwa ni  lazima uwe na wapenzi wengi

(iii) Kutumia sindano , wembe mpya kila wakati .

 

 

 

 

 C    Madhara

(i) Umaskini

(ii) Vifo

(iii) Kutengana   kwa   familia

Hoja  zozote  5

 

  1. Mwanafunzi lazima  atambue  kuwa  hii  ni methali .

Msamiati _______  Tanzu  _______ matawi

 

Maelezo                       Mti ukifa   sehemu  ya  chini  ni lazima pia  ufe  sehemu   ya   juu. Maana  ya  hapa  ni  kuwa   kiongozi mwema   akiondoka  ni lazima  aliokuwa   akiwaongoza   wakorogeke   kwa   mambo   maana   jamii  isiyokuwa  na   uongozi huangamia  .

 

Matumizi                    Walioondokewa na  kiongozi   wao  kisha  wamekorogeka   wanaweza  kufarijiwa   kwa  methali   hii.

TAZ:    Insha   ina   sehemu   mbili   ambazo   sharti   zijitokeze   katika   insha  .

 

(i) Kufa  kwa  shina   ya  mti (kuondokewa   na  anayetegemewa.

(ii ) Tanzuze  hukauka   (waliomtegemea   kuteseka)  Eleza  mateso

 

  1. (i) Kidini – Hawaruhusiwi kuhubiri  katika  baadhi  ya  madhehebu  .

(ii) Kielimu – Licha  ya   kuishi katika  karne ya  ishirini  na  moja, watu  wengine

hasa wazee) bado hawaoni haja  ya  kumwelimisha   mtoto  msichana.

(iii) Baadhi ya  waajiri hubagua  wanawake. Hawapendi kuwaajiri  kwa  sababu

watakuwa   wakienda   likizoni  kila  mara  kujifungua.

(iv) Kitamaduni   – Baadhi ya  watu  bado  hawakubali   mwanamke  arithi   mali, ale

baadhi ya   vyakula   kama  mayai, kuku   n.k.

(v) Nyumbani-  Wanaume  wengi   huwadhulumu   kutokana   na  imani   kuwa   mke

lazima  apigwe .

–  Wanafanyishwa   kazi  ngumu  (kulima , kupalilia   kuvuna) wakati ambapo

waume  wao, wanapiga  tu soga .

SHIDA                                                 SULUHISHO    

 

(i)     Ukosefu wa  kazi                                –   Kujenga   viwanda

–   Kupanua  kilimo

(ii)     Umaskini                                           –   Serikali kuwapa   watu  mikopo ya

–   kuanzisha biashara ndogo ndogo  .

 

SHIDA                                                           SULUHISHO

 

(iii) Ukabila / ufisadi                                  –  Sheria   kali  zitolewe/  hatua  kali  hukuliwe.

 

(iv)  Watu  wengi  kuhamia  mijini            –   Kujenga  viwanda   mashambani  .

 

(v)  Barabara mbovu                                  –   Barabara   zitiliwe  lami

Ugonjwa    wa  ukimwi                        –   Kuwafunza  watu  chanzo   na  madhara.

SEHEMU YA TATU

USHAIRI.

 

1.   Wahenga waliyosema

Yapotea yalo mema

Wengi tunashika tama

Si hapa si Amerika

 

2.   Yawaka moto dunia

Ya Rabi tunaumia

Wanja la fujo dunia

Utunusuru Jalia

 

3.   Yawaka moto dunia

Magogo kuzidi mia

Ulimwengu wazuzua

Hutisha na kutuchusha.

 

4.   Yawaka moto dunia

Na wengi huwalemea

Yataka kuyapimia

Yatesa kupindukia

 

5.   Yawaka moto dunia

Bila taswira kutia

Huwa na mbuzi mkia

Patupu kuangukia

 

6.   Yawaka moto dunia

Ya mazigazi julia

Ghururi imejalia

Waza ukiyawazua

 

7.   Ikikutaka dunia

Na itakupalilia

Bali ikikuchukia

Wabaki kujililia

 

8.   Yawaka moto dunia

Wivu wizi na tamaa

Mafuriko nayo njaa

Vita vingi vimejaa.

Yamejiri kwa hakika

Mawi yamenawirika

Maovu mengi yashika

Yawaka moto dunia

 

Si usiku si mchana

Kwa mengi ya kutatana

Wataka kukakawana

Yawaka  moto dunia

 

Yapandisha na kushusha

Kuyatua na kutwisha

Wachache huwachekesha

Yawaka moto dunia

 

Inayo mingi mijiza

Hupotosha na kujuza

Sije kukudidimiza

Yawaka moto dunia

 

Hubwaga zani sikiza

Kujua inavyocheza

Ukose ya kupendeza

Yawaka moto dunia

 

Ni dungudungu  dunia

Yatinga na kuchachia

Na ya chumvi hutilia

Yawaka moto dunia

 

Tapaa wakulilie

Kofia wakuvulie

Tatamani ujifie

Yawaka moto dunia

 

Kuna mengi ya kuchama

Ubaguzi usokoma

Maonevu yasozama

Yawaka moto dunia.

 

  1. Maswali.
  2. Hili ni shairi la aina gani kimuundo? Tetea majibu yako.              (alama3)
  3. Ni wasia gani unaotolewa na mshairi?
  4. Onyesha maana ya mstari toshelezi ukitoa mfano mstari wowote wa shairi. (alama 3)
  5. Eleza maana ya kipokeo cha shairi hili                                                 (alama 3)
  6. Andika ubeti wa kwanza kwa lugha ya nathari                                     (alama 3)
  7. Kwa nini mwandishi anasema dunia inawaka moto? (alama 3)
  8. Andika mbinu 2 za lugha katika shairi hili na mfano mmoja mmoja. (alama 3)
  9. Andika maana ya (i)  Kukakawana                                                     (alama 4)
  10. Mazigazi                                                 (alama 2)

 

  1. Mkusanyiko wa uma, ni mpango wa jalali,

Jalali mwenye huruma, aloumba kila mwili,

Mwili wa mtu na nyama, akatia na akili,

Akili yenye kupima, la haki na la batili,

Batili haina wema, iwapo japo kalili

 

Kalili huwa imara, iwapo na kiongozi,

Kiongozi ule busara, asiye na ubanguzi,

Ubaguzi ni hasara, isofaa siku hizi,

Siku hizi za fikara, za watu wanamaizi

Kumaizi yalo bora, yasiyo na pingamizi

 

Pingamizi kuzing’owa, baina yetu raia.

Raia tukateuwa, Serikali ya jamia

Jamia tukaridhiwa, kuwa haina udhia

Udhia tukiletewa, tusiridhi vumilia

Kuvumilia kwauwa, hasa kumwasi Jalia.

 

Jalia yake hukumu, ambayo kwetu lazima,

Lazima tumheshimu, kiongozi alomwema,

Mulema kula yake kaumu, iliompa kusimama

Kusimama muadhamu, kuitimiza kalima,

Kalima iliyotimu, nami nafunga nudhuma.

 

Maswali.

 

  1. Lipe shairi hili kichwa mwafaka                                     (alama 2)
  2. Eleza muundo wa shairi hili                                                             (alama 4)
  3. Eleza maudhui yanayojitokeza katika ubeti wa tatu                         (alama 2)
  4. Andika ubeti wa kwanza kwa lugha nathari                         (alama 4)
  5. Mwandishi alikuwa na dhamira gani katika kuliandika shairi hili?   (alama 2)
  6. Hili ni shairi la aina gani?                                     (alama 2)
  7. Huku ukitoa mifano, eleza uhuru wa kishairi alioutumia mwandishi (alama 4)

 

SEHEMU YA PILI

UFAHAMU, MUHTASARI, MATUMIZI YA LUGHA

 

              Kama   kawaida  yake  , Faki  alifika  hospitali  saa kumi  na  mbili  asubuhi  . Kawaida  hii  haikuanza   zamani   sana   kwa  hakika : Imeanza   karibuni tu , toka  kitoto  chao   chanajike   kilipolazwa    hospitali  kwa  tumbo la  kuendesha.

Masika   mama-mtu  ikambidi  akikimbie    kitanda  cha  kinyumba   kulalia   kitanda  cha  hospitali  karibu na  mwanawe  . Na Faki kwa   upande  wake   ikamlazimu kutamba na jua  na  mvua  kuizumbua  riziki angalau  ya  kupeleka  mkono   kinywani.- angalau   riziki hiyo! Na  alipoipata  riziki ya  mchana  kutwa  alijifunga  kibwebwe   kuingia  jikoni  kuitayarisha  ilike  ,  kisha  kudapia   baiskeli yake  au  mwanapata   kama watu  wengine   wanavyoita   kuelekea  hospitali   kumpelekea  mama mtoto  aghalabu  muhogo  wa kupwaza  na  chai   ya  mkandaa; na  kile  kitoto  chao , maziwa na  uji

Asubuhi kila siku  ilimbidi  atoke   mapema  , kisha  ashike   njia   kuelekea  kibaruani .

Naam  , kama  kawaida  yake  , leo aliuwacha   mparapata   wake   nje  chini  ya   ngazi   pale  hospitali,  akatoa   mkoba  wenye  uji   na  maziwa   ya  mtoto  pamoja   na  muhogo   wa   kupwaza  na  chai   ya  mkandaa   ya  mama -mtoto  ,kwenye   lile   boksi   kubwa   analolifunga   kibaoni   nyuma   ya  baiskeli   yake  . Huyo Faki  akawa  anapanda   ngazi  taratibu   kuelekea   wadi   ya   watoto kumwuona   mwele   na   muuguzi  wake

Lakini  leo , kabla  hajamaliza  kuipanda  ngazi  , alisikia    ukwenzi wa   mwanamke   ambao   ulimtuturisha  moyo  . Asingaliweza   kuipotea   sauti  ya   mwanamke   huyo  ingawaje  ilitoka  kwa  ukwenzi  . Bila  shaka  ilikuwa  sauti ya   Masika   mkewe  . Na  sasa  ukwenzi  huo  uwe  wa  nini  ?  Uwe wa  nini  enh,  isipokuwa  ……….

Alitimka, akazipanda  ngazi   kwa  vidato  vitatu  vitatu. Macho  yakamtoka na  moyo  ukamhaha  . Joto la  ghafla  likamjia.  Na  hofu ikamjaa. Huyo kufumba  na kufumbua, alijkuta   katika  mbele  ya  Masika   mkewe   aliyekuwa  kashikiliwa   vyema   na  wauguzi ;   wengine  kulia  na wengine  kushoto  huku  akiwawa  na   kupiga makambi  na  mayowe  .

 

“Nini ?” Alibwata Faki  pale alipokuwa kasimama kama shujaa aliyechomwa sime na  kuyasikiliza  maumivu. “ Mwanangu …….” Alipayukwa  Masika, “ maskini damu yangu …  mume  wangu  ewe   mwenzangu…… nguvu  zetu, jasho letu, mtoto …….aaaa  mama! Uchungu wa mwana unauma! Tumbo linanikeketa !” Aliendelea  kulalama   Masika.

Lugha  hiyo  ilitosha  kujibu  swala la  Faki   lililomwenda   akilini.  Kila  kitu  kilikuwa  wazi.  Faki  sasa alikwisha   maizi   nini  kimetokea. Hima alipiga  goti  chini   kufikia  kimwili  kilichozongwa  shiti  jeupe   na  kulazwa  kigodononi sakafuni. Huku  mwili   mzima   ukitetema, taratibu  alinyoosha  mikono  kukiteka   hicho   kijimwili   kisha   aliinuka   na  kwenda  nacho  kwa  mkewe.

“ Mume  wangu, haaikuwa  riziki  yetu …..”  aliendelea  kulia   Masika

“Nyamaza   Masika”,  alitamka   Faki   kwa   upole  huku    akijaribu    kuyazuia   machozi  yaliyokuwa  njiani  . “ Kila  liandikwalo   halina   budi kuwa, lazima  ….”

alishindwa     kuyamaliza  aliyotaka   kuendelea   kuyasema .

 

Maswali.

 

(a)   Eleza  kwa nini   Faki alikuwa  akienda  hospitali  kila   siku                  (alama 2)

(b)   Taja  jina  lingine  lililotumiwa  katika  taarifa   kurejelea   baiskeli     (alama 1)

  1. c) Kwa  nini  Faki alilazimika  kutafuta kibarua  kila  asubuhi                   (alama 3 )

(d)   Eleza  sababu  iliyomfanya   Masika   kupigwa  ukwenzi                       (alama 2)

(e)  Unadhani  mwandishi   ana   maana   gani  anaposema, “……ilitosha  kujibu  swala

la  Faki  lililomwenda   akilini  kila  kitu kilikuwa  wazi”                        (alama 3)

(f)   Fafanua  maana  ya, “ mume  wangu   haikuwa  riziki yetu ……”          (alama 3)

Taja  maneno   yoyote   mawili   kutoka   kwa  taarifa   ambayo yamefanyiwa utohozi  kutoka  lugha  ya   kiingereza                                                         (alama 2)

(h)   Eleza  maana   ya ;                                                                                   (alama 4)

Alijifunga  kibwebwe

Machozi  yaliyokuwa  njiani

UFUPISHO.

 

  1. Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali

 

Ninashukuru   wanafunzi wote   wa  dasara   langu  kwa  kuhudhuria   mkutano   huu  nilioitisha  dakika  ya mwisho. Najua   walimu   washaanza  kukata vipindi  vyote baada   ya kumaliza   mambo yaliyohitajika   kufunza  toka   juzi.  Na  sasa  mmepewa   nafasi   kubwa   ya  kujitayarisha   vizuri  zaidi  kwa  ajili  ya  mtihani  wenu   wa  mwisho, lakini  mimi  nimeona   kwamba  upo  muhimu   wa  kuzungumza   na  nyinyi  katika  dakika hii  ya  mwisho. Madhumuni  si  kufunza  zaidi, maana  hakuna   tulichosaza   kwa  mujibu  wa  muhtasari  wa   masomo   lakini  ninataka   kuwapeni  maoni   yangu ya mwisho  kabisa .  Hasa   nitawaeleza   yale  ya  kuzibia   nyufa   ndogondogo  zilizobaki  na  pia kuwafunulia   kunga  za  maisha  ambayo  wengine   mtalazimika   kuyakabili   kwani   ingawa  sote   tunawatakia   heri mufaulu  mtihani na   hatuna  shaka   mtafaulu, yawezekana   kwamba   mtapata bahati  mbaya  katika   mtihani   na   mlazimike   kujiunga   na  maisha  moja   kwa  moja.

Kwa  kuwa  tumefika  ukingoni   mwa  safari  yetu  tuliyoianza   miaka  minne   iliyopita,  ninataka  kuwapigia  kengele ya   mwisho. Hapa  ninazo karatasi  zenu za majaribio  mliyoyafanya  juma lililopita. Nina  furaha   kusema  ya kuwa   nyote mmejaribu maswali kama  ilivyostahili.  Hata  hivyo  msivimbishe  vichwa   mkaja  mkachafua   mambo dakika   ya  mwisho katika   mitihani  yenu. Wahenga  wamesema, mgema  akisifiwa  tembo  hulitia  maji.  Kumbuka  hilo jaribio  si mtihani   wa  mwisho,  kazi bado ingalipo  na inakukodoleeni   macho  .Pengine  si  vizuri  kwa  wakati   huu  kusoma  sana   na  kukesha, lakini  ni wakati  wa kuzipiga  brashi   na  kuzisafisha zile   sehemu ambazo   kila moja  wenu   anaziona   hajazipitia   vizuri , au hazijui  vizuri  au  hajaziwekelea  uzito. Zidini  kujitayarisha   vyema,   zaidi  na  zaidi. Mkifanya  hivyo, kila kitu   kitakuwa   wazi   kwenu na   mtaiona  faida   ya  kazi   na uvumilizi  wenu.

Ningependa   kusema   kwamba   sasa  ninaosha  mikono  yangu   kabisa   sina  ambacho   ni cha lazima   sijawafunza.  Baadhi ya  mengi   mjuayo  yatatahiniwa  lakini   mengine hayatatahiniwa   kwani kutunga mtihani   si kuandika   kitabu ,  bali ni kutunga   maswali  ya kupima  kama  unajua  mengi uliyofundishwa . Hata   hivyo, kwa  kuzijua  nyanja   zote  za  kiswahili  zilizopendekezwa   kwenye   muhtasari   wa  masomo,  hakuna  kitakacho kushindeni.

Naomba  myakumbuke   maaso  yote  niliyowapa na  jinsi  ya kukabiliana   na mitihani na hata  ulimwengu  wenu . Endeleeni  na   bidii  yenu. Na  hili la  ulimwengu wenu  ndilo la  muhimu   sana.  Maana  ya  kufanikiwa katika  mtihani  si kufanikiwa  na    maisha.  Maisha  yanataka  mbinu zake.  Mnakokwenda nje  ya  kuta  za  darasa   kuna  ulimwengu,  na  wazee  wamesema, asiyefunzwa  na  mamaye   hufunzwa  na  ulimwengu.   Ulimwengu  msiuingie   kwa  hamu na  pupa   na kutaka  kuyavamia  yale   yote  ambayo  mlikuwa  mkiyakosa   mlipokuwa   shule.  Mkitaka  kufikisha   kisugudi kabla  vidole  havijafika, mjuwe  huenda   mkavunja  mikono   yenu.

Ulimwengu una  mengi ya  kuvutia, lakini si kila  zuri na  la kuvutia   ni zuri katika  hakika   yake. Vyengine  vinang’ara, lakini si dhahabu. Na  isitoshe  si kila  mtu miongoni mwenu  ana  uwezo   wa kupata  kila   anachokitaka. Lazima  wengine  miongoni  mwetu  tujikune  tujipatiapo. Tusiwaige  watu  ambao  tunajua   ukunjufu  wao  wa  matumizi  ulivyo. Hakika   mwiga   tembo  kumeza  boga, huchanika   msamba.

Lazima   katika   dunia  ya leo  uishi pamoja   na  watu  – yaani usijitenge, bali  shirikiana   na  wenzako   kwani  ulimwengu wa  siku hizi  ni ulimwengu wa  mtu kumtegemea mwenzake, hata  ikawaje.  Mheshimu  anayekuheshimu, mfundishe  heshima   asiyekuheshimu . Wapende  wazee  wako, majirani  zako, na  zaidi ipe nchi yako  nafsi yako.Ukipata  kazi ithamini kazi yako, maana  siku hizi   kazi  si kitu cha kuchezea .Kama  hukupata  kazi ya  kuajiriwa,tumia  akili ,busara  na maarifa yako kujitegemea  .Mengi mmefundishwa   katika mfumo wa  elimu   wa  8 : 4 : 4 ili mjitegemee.  Si rahisi tena   serikali kumpa kila   mtu kazi. Usitahimilivu ni msingi  wa  maendeleo. Jengo  halisimami   kwa  siku  moja, lataka  idili  ya  mchwa.

Hii  sasa  ndio  hatima  ya mimi   kuwa nanyi kama   mwalimu wenu  wa  kidato hiki na nyinyi  ndio mwisho   kuwa   wanafunzi  wangu. Tuna  mengi ya  kukumbuka. Tusisahau  uhusiano   wetu. Zaidi  na  watakia  kila  la  heri  katika  mitihani   yenu na  maisha  kwa  ujumla .

 

(a)  Eleza mambo muhimu  katika  aya  ya pili            ( maneno  50- 60 )      (alama 7)

(b)  Eleza  maaso ambayo  wanafunzi walipewa katika   aya  ya nne.  ( maneno   65-75)                                                                                                                 (alama 9)                                                                        

(c)   Mwalimu  alitoa  maaso  gani   kwa  wanafunzi  iwapo hawangebahatika  kuajiriwa ?

(maneno  35-40)     (alama 4)

 

MATUMIZI  YA LUGHA . 

 

  1. (a) Ainisha sentensi hizi                                                                (alama  4)

Maji             ukiyavulia           nguo               yaoge

Twende       kwetu                 sasa hivi

 

(b)  Taja  vielezi   vinavyopatikana katika  sentensi   hizi ; kisha  eleza ni  vielezi 

     vya  aina   gani.                                                                                        ( alama 4 )

(i) Anafanya  kazi  kwa   mwajiri  wake  .

(ii) Alifanya   mambo  kisirisiri.

 

(c)  Toa  jibu moja   sahihi   linalooana   na  tungo   ulizopewa                (alama 2)

(i)  Mabaki ya jengo lililobomoka  au  mtu  aliyekonda  kupita  kiasi

(ii) Sehemu ya pwani  ambayo  meli   hufungwa   ili kupakia   shehena

 

(d)  Sahihisha    sentensi   zifuatazo                                                              (alama 4)

(i) Uko  na  pesa  yoyote unikopee  ili  niweze kukidhi  mahitaji yangu ?

(ii) Yule  msichana  anijiringa  tu  bila   kujua   kuna   kuringa  hiyo   haitamsaidia  sana  .

 

(e) Taja  kinyume  cha   kila  mojawapo  ya  maneno  yafuatayo          (alama 4)

(i)  Kudai

(ii) Unganisha

 

(f) Unda  majina  mawili  kutokana  na kila   kitenzi  ulichopewa        (alama 4)

(i)  Tatua

(ii) Kunja

 

(g)  Eleza  maana  ya  semi   hizi                                                                    (alama 4)

(i)   Kata   kalima

(ii)  Kuzua maneno

 

 

(h) Andika upya  sentensi   hizi  bila kutumia  neno amba                          ( alama  4)

(i)  Ugonjwa  ambao ni hatari  sana  ni ukimwi .

(ii) Nilimwona  simba  akinyemelea  banda   la  ng’ombe   nilipokuwa  nikishika   zamu

Kanusha  sentensi hizi .                                                                     ( alama 2 )

(i)   Nitaenda  bungeni   alasiri  kuhudhuria   kikao .

Tumesimama  hapa  sana  .

 

(k) Andika  maneno haya  katika hali ya   kufanyiana                              ( alama 2 )

(i) Soma

(ii) Iba

 

(l) Huyu  ni nani?                                                                                           ( alama  1)

(i)  Mwamu

(ii) Kamilisha methali  ifuatayo                                                                (alama 1) .

(iii) Mkataa  wengi  __________________________________________________

 

SEHEMU YA PILI

MWONGOZO  WA  KUSAHIHISHA

UFAHAMU, MUHTASARI, MATUMIZI YA LUGHA

 

1.   UFAHAMU

  1. Alikuwa akienda  hospitali kila siku kwa  sababu  mtoto  wake msichana  alikuwa amelazwa huko .

(b)   Mparapata

(c)  Alilazimika  kutafuta    kibarua  ili   apate  pesa   ya  kununua  chakula  chake mwenyewe   pamoja  na  mkewe  na  mtoto.

(d) Masika alipiga  ukwenzi kwa sababu  mtoto wake aliyelazwa  hospitalini  aliaga

dunia

(e) Ina maana kuwa Faki alifahamu sababu  ya mkewe kulia  ilikuwa kifo cha mtoto

wao.

(f) Masika   alimaanisha   kuwa  mungu   hakuwa   amepanga    mtoto  huyo

angeishi .

(g) Wadi

Shiti

(h) (i) Alifanya kazi kwa bidii

  1. ii) Alikuwa karibu  kulia  .

 

  1. UFUPISHO

(a)

(i)  Wanafunzi wasivimbishe  vichwa , wakaja  wakachafua  mambo  dakika  ya mwisho.

(ii)  Jaribio  si  mtihani  wa  mwisho  , bado  kazi   ingalipo  na  inakukodoleeni  macho.

(iii) Si  vizuri wakati huu  kusoma  sana  na kukesha  lakini   ni wakati wa ; Kuzipiga  brashi  na kuzisafisha

sehemu ambazo  kila mmoja  wenu  anaziona  hajazipitia   vizuri.

(v) Zidini  kujitayarisha   vyema   zaidi  wa  zaidi .

 

 

(b)

(i) Endeleeni na  bidii  yenu

(ii) Kufanikiwa  katika  mtihani   si kufanikiwa  katika  maisha.

(iii) Asiyefunzwa  na mamaye, hufunzwa  na  ulimwengu  .

Msiuingie  ulimwenguni  kwa hamu   na pupa  na kutaka kuyavamia yale yote

ambayo  mlikuwa  mkiyakosa mlipokuwa  shule.

(v)  Ulimwengu  una mengi   na  kuvutia , lakini  si kila  zuri na la  kuvutia, ni zuri

kwa hakika  yake

(vi) Si  kila mtu  miongoni  mwenu  ana   uwezo  wa  kupata  anachokitaka.

(vii) Tusiwaige  watu  ambao  tunajua  ukunjufu wao  wa  matumizi  ulivyo.

{m—— 7}

                                                   {u——–2}

                                                                  9

 

  1. c) (i) Tumia akili, busara na maarifa  yako kwa

(ii) Mengi mmefundishwa  katika mfumo  wa  elimu  wa   8: 4: 4  ili   mjitegemee

(iii) Si rahisi tena   serikali   kumpa   kazi  kila   mtu.

{m——3} 

                                                  {u ——1} 

                                                               4

 

  1. MATUMIZI YA LUGHA

(a)

(i)  Maji                  ukiyavulia               nguo                    yaoge

Kiima                Kitenzi                   Kitendewa           Kitenzi

 

(ii)  Twende                  Kwetu                                          Sasa hivi

Kitenzi                   Kivumishi                                    Kielezi

Kimilikishi

 

(b)(i)  Kwa  – kielezi  cha  mahali

(ii) Kisirisiri  – kielezi  jinsi  / namna

 

  1. c) (i) Gofu

(ii)  Gati

(d) (i)  Una  pesa  zozote  unikopeshe  ili  niweze   kukidhi  mahitaji yangu ?

(ii) Yule msichana  anaringa  tu  bila kujua  ya  kuwa  maringo  hayo  hayatamsaidia

sana

(e) (i) Kudai –  Kulipa

(ii) Unganisha  –  tenganisha

(f) (i) Tatua  – utata  , tatizo ,  kutatana  , mtatizi    (yoyote  mawili)

(ii) Kunja  – Mkunjo  , ukunjaji, kukunja ,         (yoyote mawili)

(g) (i) Kata   kalima  –  Acha  kusema  ghafla

(ii) Kuzua   maneno – kusema  uwongo .

(h) (i) Ugonjwa  ulio  hatari sana   ni ukimwi .

(ii) Mtumwe  aliyepigwa  na  mawe  alikuwa  Stefano .

(I) (i)  Ka   imetumika  kuonyesha  matendo  yanayofuatana   kwa  kutendeka  kwa

wakati uliopita

(ii)  Ki    imetumika  kuonyesha  kuwa ,kitendo  kilikuwa  kikiendelea wakati ambapo

kingine kilikuwa  kikitendeka.

 

(j)  (i)  Sitaenda   bungeni   alasiri  kuhudhuria  kikao.

(ii)  Hatujasimama  hapa  sana  .

(k)  (i) Soma  – Someana

(ii) Iba     – Ibiana

(l) (i) Mwamu –   Shemeji   wa  kiume .

(ii) Mkataa wengi    ni  mchawi                                                                                   

Comments

5 responses to “KISWAHILI NOTES- REVISION KIT”

  1. سئو سایت یعنی چه Avatar
    سئو سایت یعنی چه

    Howdy! This is kind of off topic but I need some help from
    an established blog. Is it very difficult to set up your own blog?
    I’m not very techincal but I can figure things out pretty
    quick. I’m thinking about setting up my own but I’m
    not sure where to start. Do you have any ideas or suggestions?
    With thanks

  2. Dr Marie Avatar
    Dr Marie

    Je! unataka kununua figo, viungo vya mwili au unataka kuuza yako
    figo au viungo vya mwili? Je, unatafuta fursa ya kuuza
    figo yako kwa pesa kutokana na kuharibika kwa kifedha na hujui la kufanya, basi wasiliana nasi leo na tutakupa kiasi kizuri cha pesa $500,000 dola kwa Figo yako. Jina langu ni Daktari Patricia Marie na mimi ni Daktari Bingwa wa Mishipa ya Fahamu katika MAX HEALTH CARE Hospitali yetu ina utaalam wa Upasuaji wa Figo na pia tunashughulika na ununuzi na upandikizaji wa figo na wafadhili anayeishi na sambamba. Tunapatikana India, USA, Malaysia, Singapore. Japani.

    Tafadhali tujulishe ikiwa una nia ya kuuza au kununua figo au
    Organs tafadhali usisite kuwasiliana nasi kwa na kupitia barua pepe.

    Barua pepe: [email protected]

    Kila la heri
    MKURUGENZI MKUU WA TIBA

  3. Visit Website Avatar
    Visit Website

    Hello my friend! I want to say that this article is amazing, nice written and include almost all important infos. I would like to look more posts like this .

  4. عطر مردانه Avatar
    عطر مردانه

    It’s very effortless to find out any matter on web as
    compared to textbooks, as I found this piece of writing at this site.

  5. gigantic Avatar
    gigantic

    Thankѕ a bunch for sharing this with all people
    you really recоgnisе what you’re speaking apⲣroximately!

    Bookmarked. Кindly additionally talk over with mү website
    =). Wе can have a hyperlink change arrangement between us

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

TRENDING NOW

Search THIS SITE.

Are you a teacher, a student or Parent? Download free Education Resources here.